*************
Na Mwandishi
Wetu
MKUU wa wilaya ya Ilala
Raymond Mushi amewasisitiza wadau mbali mbali kuwekeza katika mpira wa miguu
kwani hutoa ajira nyingi kwa vijana na kuwafanya wajipatie
kipato.
Akiongea na waandishi wa
habari baada ya kufunga mashindano ya Bonnah Cup yaliyoandaliwa na diwani wa
kata ya Kipawa Bonnah Kaluwa, Mkuu wa wilaya alisema kuwa kwa miaka ya sasa
mpira umekuwa kimbilo kubwa la ajira kwa vijana kwani huweza kuwasaidia
kujiingizia kipato.
Mushi alisema kuwa pamoja
na wadau kuwekeza katika mpira wa miguu, Tanzania itaweza vile vile kukuza
vipaji ambavyo huwa vinapotea.
“Tanzania tuna vipaji
vingi sana vya mpira wa miguu, tatizo ni vipaji hivyo kuvumbuliwa hivyo
nawaombeni wadau mbali mbali kutoka sekta zote kujitokeza kuweza kuwekeza katika
tasnia hii, ambapo tutawezesha vijana wetu kujipatia ajira,”
alisema.
Timu ya Stakishari kutoka
Mogo iliifunga timu ya Vipaji Halisi kutoka eneo la airport katika fainili na
kukabidiwa kombe pamoja na kiasi cha shilingi laki tano, ambapo mshindi wa pili
alipata kiasi cha shilingi laki tatu na mpira moja na mshindi wa tatu alipata
shilingi laki moja na mpia.
Jumla ya timu 20 kutoka
katika kata ya kipawa zilishiriki katika mashindano
hayo.
Muandaaji wa mashindano
hayo diwani wa kata ya Kipawa Bonnah Kaluwa alisema “Lengo kubwa ya kuandaa
mashindano haya ni kuwaleta vijana pamoja iliwaweze kufahamiana na kushirikiana
lakini pia kuinua vipaji vya vijana katika mchezo wa mpira wa miguu.
Vijana wengi wanaocheze
katika ligi hapa nchini wamechipukia katika kata ya Kipawa. “ Napenda
kuendeleza na kukuza vipaji wa vijana iliwaweze kufikia kiwango cha juu zaidi
katika mchezo huu”, alisema
Said Mkuwa,
Mwenyekiti wa mashindano hayo aliongezea: “Tunamshukuru sana diwani kuandaa
mashindano haya kwa ajili ya vijana, alisema “Nimefurahi
kwamba mashindano yamekwenda vizuri tangu mechi za mwanzo hadi fainali na vijana
wameshirikiana vizuri katika michezo yote”
Comments