Dola Bilioni 1.1 kujenga upya Nigeria
China imekubali kutoa mkopo wa
dola bilioni 1.1 kwa Nigeria ili kufadhili ukarabati wa miundo
msingi.Mkataba huu umeafaikiwa wakati wa ziara ya Rais Goodluck Jonathan
mjini Beijing,ambapo alikutana na mwenyeji wake Xi Jinping.
Nigeria inaongoza kwa kuzalisha mafuta Afrika lakini kwa miaka imekua na miundo msingi mibovu, huku mamilioni ya raia wake wakiishi kwa umasikini. Bw. Xi amesema nchi mbili zinashirikiana kwa minajili ya kuboresha maisha ya watu wake.
Rais Jonathan anaongoza ujumbe wa wawekezaji wa Nigeria huko China na ziara ya siku nne itasaidia kuleta mshikamano wa karibu wa kibiashara.
Kampuni za ujenzi za Ki-China zimeanza kujenga barabara nchini Nigeria, kwa kandarasi ya dola bilioni 1.7.China kwa upande wake inatarajia kupata mapipa laki mbili ya matufa ghafi kutoka Nigeria ifikapo mwaka 2015.
Comments