Dola Bilioni 1.1 kujenga upya Nigeria

Viongozi wa Nigeria na China mjini Beijing

China imekubali kutoa mkopo wa dola bilioni 1.1 kwa Nigeria ili kufadhili ukarabati wa miundo msingi.Mkataba huu umeafaikiwa wakati wa ziara ya Rais Goodluck Jonathan mjini Beijing,ambapo alikutana na mwenyeji wake Xi Jinping.

Fedha hizi zitasaidia ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege na kujenga miji minne na njia mpya ya reli.China inawekeza kwa kiwango kikubwa Barani Afrika ambapo pia imekua ikipata raslimali za mafuta na madini.

Nigeria inaongoza kwa kuzalisha mafuta Afrika lakini kwa miaka imekua na miundo msingi mibovu, huku mamilioni ya raia wake wakiishi kwa umasikini. Bw. Xi amesema nchi mbili zinashirikiana kwa minajili ya kuboresha maisha ya watu wake.

Rais Jonathan anaongoza ujumbe wa wawekezaji wa Nigeria huko China na ziara ya siku nne itasaidia kuleta mshikamano wa karibu wa kibiashara.

Kampuni za ujenzi za Ki-China zimeanza kujenga barabara nchini Nigeria, kwa kandarasi ya dola bilioni 1.7.China kwa upande wake inatarajia kupata mapipa laki mbili ya matufa ghafi kutoka Nigeria ifikapo mwaka 2015.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*