Hali ya Mandela imeimarika asema Bi. GRACA
Mke wa Nelson Mandela, Graca
Machel amesema kwa sasa hana wasi wasi sana kuhusu afya ya rais huyo wa
zamani wa Afrika Kusini kama ilivyokuwa wiki chache zilizopita.
Bi Machel amesema hali ya Mandela inaendelea kuimarika kila uchao.Mandela ambaye ni rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, mwenye umri wa miaka tisini na nne, anasemekana kuwa katika hali mahututi.
Mandela alilazwa hospitalini wiki tano zilizopita na hapo jana rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, alisema kuwa mwanaharakati huyo wa uhuru amesalia kuwa mpiganiaji mkubwa kama alivyokuwa miaka hasmini iliyopita.
Comments