MKUTANO MKUU WA WANACHAMA WOTE

 
MWENYEKITI wa Simba, Mhe; Ismail Aden Rage, anawakaribisha wanachama wote wa Simba katika Mkutano Mkuu wa Wanachama utakaofanyika kesho katika bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo ni wa kawaida wa kila mwaka na unaendeleza utaratibu wa uongozi wa Alhaji Rage kufanya mikutano kama hiyo kwa kadri Katiba ya klabu inavyotaka.

Ikumbukwe kuwa katika miaka ya nyuma, kuna kipindi klabu haikuwa ikifanya mikutano kama hii kwa kipindi kirefu na hivyo huu ni utaratibu mwafaka katika kuendeleza klabu ya SIMBA.

Kwa mwaliko huu, Mwenyekiti anawataka wanachama wote walio hai kuhudhuria mkutano huo na KLABU INASISITIZA KWAMBA WANACHAMA AMBAO HAWATAKUWA HAI HADI ASUBUHI YA SIKU YA MKUTANO HAWATARUHUSIWA KUINGIA MKUTANONI. HII MAANA YAKE NI KWAMBA WANACHAMA HAWARUHUSIWI KULIPIA KADI ZAO KWENYE ENEO LA MKUTANO SIKU YA MKUTANO.

Mkutano unatarajiwa kuanza saa tatu kamili asubuhi na wanachama wote wanaombwa kujali muda.
Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utapokea na kujadili Ripoti ya Mapato na Matumizi ya Klabu kwa mwaka ulioisha kama ilivyokaguliwa na wakaguzi wa hesabu, kupokea taarifa ya Mpango Mkakati wa Klabu (Strategic Plan) ulioandaliwa na maprofesa wa Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT).

MECHI YA SIMBA NA URA

TIMU za Simba na URA ya Uganda zimewasili jijini Dar es Salaam tayari kabisa kwa pambano la kesho katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Pambano hilo litakuwa la kwanza kwa Simba kucheza kwenye uwanja huo tangu kumalizika kwa Ligi Kuu ya Tanzania na ikiwa imetoka katika ziara ya mafanikio ya mikoa ya Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini.

URA imewasili jijini jana ikiwa na msafara wa wachezaji 23 na viongozi sita. Baadhi ya wachezaji maarufu waliokuja na timu hiyo ni Derick Walulya, George Owino na Musa Doca.
Pambano hilo litaanza majira ya saa kumi kamili jioni.

MSIBA
KWA niaba ya Kamati ya Utendaji ya Simba, Wanachama na Wapenzi wa klabu, Mhe; Rag anatoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Mzee Juma Urongo aliyefariki dunia asubuhi ya leo na kutarajiwa kuzikwa leo jioni huko Tandika jijini Dar es Salaam.

Mzee Urongo alikuwa miongoni mwa wajumbe wa Baraza la Wazee la Simba na ni miongoni mwa kizazi cha wazee walioanza kuishabikia klabu tangu ikiitwa Sunderland.

Rage amesema binafsi atakosa sana busara, ushauri na maelekezo yam zee huyo ambaye alikuwa shabiki wa Simba katika nyakati nzuri na mbaya.

Mungu na aiweke mahali pema roho ya marehemu Juma Urongo.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.