Murray bingwa mpya wa Wimbledon

Andy Murray
Andy Murray amekuwa Muingereza wa kwanza kushinda taji la Wimbledon tangu mwaka 1936, ikiwa ni zaidi ya miaka 77.
Murray amemfunga Novak Djokovic raia wa Serbia kwa seti tatu kwa kwa bila katika mchezo wa fainal za wanaume za michuano ya tenesi ya Wimbledon.
Murray amemshinda mchezaji anayeorodheshwa wa kwanza duniani Novak Djokovic kwa seti tatu kwa bila za 6-4, 7-5, 6-4.
Andy Murray amesema anashindwa kuamini kile alichokifanya kwani mechi hiyo ilikuwa ngumu, huku joto likiwa kubwa lakini anashukuru ameweza kumaliza mechi hiyo kwa ushindi muhimu kwake na kwa taifa.
Hili ni taji la pili la michuano mikubwa ya tenesi duniani maarufu kama Grand Slam baada ya kushinda lile la Michuano ya wazi ya Marekani.
Muingereza wa mwisho kushinda taji la Wimbeldon ambalo hufanyika mjini London kila mwaka alikuwa ni Fred Perry aliyeshinda taji hilo kwenye michuano ya mwaka 1936.
Mwaka jana Andy Murray alipoteza mchezo wa fainali ya michuano ya Wimbledon kwa kufungwa na Roger Federer.
Malkia wa Uingereza, Elizabeth wa pili amemtumia ujumbe wa Pongezi Andy Murray kwa ushindi wake katika mechi ambayo ilishudiwa pia na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameroon.
Bofya Maelezo zaidi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*