Mzozo wa familia ya Mandela watokota




Mandla Mandela
Mjuu wake Nelson Mandela, Mandla , amewatuhumu jamaa zake kuwa na njama ya kutaka udhibiti wa mali ya babu yake rais wa zamani wa Afrika Kusini.
Matamshi yake yanakuja baada ya mahakama kuamuru kuwa mabaki ya wanawe Mandela kufukuliwa na kuzikwa nyumbani kwa Mandela katika kijiji cha Qunu.
Mnamo Jumatano polisi walifukua mabaki ya wanawe Mandela nyumbani kwa Mandla kufuatia agizo la mahakama baada ya kuwasilisha malalamiko yao mahakamani.
Mandela, mwenye umri wa miaka 94, yungali hali mahututi hospitalini lakini madaktari wamedhibiti hali yake.
Rais Jacob Zuma alitoa taarifa baada ya kumtembelea mzee Mandela hospitalini mjini Pretoria.
Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya familia ya Mandela juu ya urithi wake lakini imekithiri huku hali yake ya kiafya ikiendelea kuwa mbaya zaidi.
Mzozo huu wa hivi karibuni kuhusu makaburi unatokana na hoja ya wapi azikwe Mandela akifariki.
Stakabadhi zilizowasilishwa mahakamani wiki jana zilionyesha kuwa anatumia mashine ya kupumua.
Alilazwa hospitalini tarehe 8 mwezi Juni baada ya kuugua maradhi ya mapafu.
Mkewe amesema kuwa Mandela wakati mwingine anasumbuka lakini hajalalamika kusema anahisi uchungu wowote.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI