"Nelson anapata nafuu", Zuma
Nelson Mandela anaendelea kupata
nafuu, licha ha afya yake kuendelea kuwa mbaya. Hii ni kwa mujibu wa
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, baada ya kumtembelea hospitalini. Rais
huyo wa zamani amelazwa hospitalini ambapo anamatatizo ya kupumua.
Rais Zuma amewaomba raia wa Afrika Kusini
kuendelea kuonyesha mapenzi yao kwa Mzee Madiba.Kiongozi wa jamii ya
Thembu, Mfalme Buyelekhaya Dalindyebo aliambia shirika la habari la AFP
kwamba Mandela alikua na fahamu alipomtembelea hospitalini.Wiki jana Rais Zuma alikanusha taarifa kwamba Mandela alikuwa hali mahututi. Shujaa huyo wa kupinga ubaguzi wa rangi Afrika Kusini alifungwa jela miaka 27 na kuachiwa huru mwaka 1990. Alichaguliwa Rais mwaka wa 1994 na kuhudumu kwa muhula mmoja pekee.
Comments