NJIWA ATUMIKA KUTOA VITISHO MAMLAKA YA RELI MKOA WA MBEYA
Njiwa akiwa na ujumbe wa barua kama inavyo
anavyoonekana
Njiwa akiwa amedhoofu kwa Baridi akiwa katika choo cha
wanaume
Barua iliyoletwa na Njiwa maeneo ya Ofisi ya Mwajiri
upande wa mbele na nyuma.
Stesheni ya TAZARA kituo cha
Mbeya
PICHA ZOTE NA MBEYA YETU.
WAFANYAKAZI wa Mamlaka
ya Reli, kati ya Tanzania na Zambia(TAZARA) jana walijikuta katika wakati mgumu
na baadhi yao kulazimika kuzikimbia ofisi zao, baada ya ndege aina ya njiwa
kukutuwa katika moja ya choo cha ofisi hiyo akiwa amefungwa hirizi shingoni,
huku akiwa na barua yenye ujumbe wa onyo kali.
Tukio hilo la aina
yake, lilitokea mapema leo saa mbili asubuhi katika ofisi za mamlaka hiyo
zilizopo eneo la Iyunga Mkoani hapa, hali ambayo mbali na baadhi ya wafanyakazi
wake kuzikimbia ofisi, ilisababisha kuibuka kwa mjadala mkubwa dhidi ya tukio
hilo.
Mtandao huu ulifanikiwa
kushudia njiwa huyo mweusi akiwa nyuma ya choo cha kiume katika eneo hilo la
ofisi ya mwajiri, huku akiwa amefungwa hirizi shingoni iliyozungushiwa shanga
mchanganyiko wa rangi tatu, ambazo ni Nyekundu, Njano na
Nyeupe.
Mbali ya kuwa na hirizi
hiyo, pia njiwa huyo alikuwa amebeba barua inayodaiwa kuwa ni ya mmoja wa
wafanyakazi wa Mamlaka hiyo (jina limehifadhiwa kwa sababu maalumu) ambaye
anadaiwa hivi karibuni kufukuzwa kazi kwa makosa ya
ubadhirifu.
Barua hiyo ilikuwa na
maandishi mekundu yenye ujumbe ulioandikwa kwa lugha mbili za Kiswahili na
kiarabu, ambapo katika maandishi ya Kiswahili yalisomeka “ Naomba majibu haraka
kama mtarudisha binti huyu kazini” ilisema sehemu ya ujumbe huo, huku ikiwa na
orodha ya majina matatu ya viongozi wa shirika hilo.
Mbali na ujumbe huo
ukiwa umeandikwa kwa maandishi ya mkono yaliyokolezwa kwa wino mwekundu upande
wa nyuma, lakini upande wa mbele kulikuwa na maandishi yakiwa ni barua ya
kutaarifiwa kufukuzwa kazi kwa mfanyakazi huyo.
Akizungumzia tukio
hilo, Mwajiri wa mamlaka hiyo kanda ya Mbeya, aliyejitambulisha kwa jina la
Mchaba Mgweno, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba waliobaini ni wahudumu
wa usafi.
Aliongeza kuwa baada ya
kupokea taarifa hiyo aliwaarifu na wafanyakazi wenzake ambao walikusanyika na
kumshuhudia Njiwa huyo mweusi akiwa amedhoofika huku akiwa na barua hiyo yenye
vitisho.
Alisema baada ya
kushuhudia hali hiyo waliamua kutoa taarifa kituo cha polisi kilichopo ndani ya
shirika hilo, ambapo waliichukua barua hiyo na baadhi ya wafanyakazi hao
wakienda kutoa maelezo kituoni hapo.
“Kwa kweli hali hii si
ya kawaida, ila kwa sasa siwezizungumzia chochote kwa kuwa hata mimi tukio hili
limeniweka katika wakati mgumu na nimeshindwa kuendelea na majukumu yangu ”
alisema Mgweno.
Hata hivyo kuliibuka
malumbano makali kati ya wafanyakazi wa shirika hilo walioshuhudia tukio hilo,
ambapo baadhi yao wakidai kuwa tukio hilo ni la kutengenezwa kwa lengo la
kuchafuana.
“Hebu angalia hiyo
barua yenyewe mbona ni kivuli (Photocopy), kama ingekuwa ni ya ….wanamtaja
mfanyakazi aliyefukuzwa jina limehifadhiwa ingekuwa ni nakala
halisi….haiwezekani mambo haya ni kutaka kuchafuana tu” alisema mmoja wa
wafanyakazi hao.
Lakini baadhi yao
wakiamini kweli kuwa barua hiyo ilitumwa ili itoe vitisho kwa viongozi wa
shirika hilo.
Baadhi ya askari polisi
wa kituo cha Tazara walikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na
uchunguzi ili kubaini ukweli wake.
“Ndugu zangu nyie
mnajua taratibu za utoaji wa taarifa kwa jeshi hili, maana wapo wahusika, lakini
kwa kifupi sisi tulipokea taarifa na tunaendelea kuzifanyia kazi” alisema mmoja
wa askari hao.
Hata hivyo, hadi
tunapoondoka eneo la tukio majira ya saa sita mchana Njiwa huyo alikuwa bado
yupo eneo la tukio.
Comments