NMB
kwa kupitia idara yake ya biashara za Kilimo (Agribusiness Department) leo
imetoa ripoti mbili;
1.
Utafiti wa kujua kama mfumo wa stakabadhi mazao ghalani (Warehouse
Receipt Financing Sytem) una manufaa kwa wakulima au la? Utafiti umethibitisha
kuwa mfumo una manufaa kwa wakulima japokuwa kuna changamoto bado. Mfano
wakulima wa kahawa wanaouza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani
wanapata zaidi ya asilimia 30% ukilinganisha na wale wasiotumia mfumo wa
stakabadhi ghalani.
2.
Utafiti wa sekta ya sukari unaonesha kuwa Tanzania inatumia wastani wa
tani 520,000 kwa mwaka (ikiwemo sukari kwa matumizi ya viwanda) kati ya hizo
uzalishaji ni tani 300,000 na kiasi cha tani 220,000 zinaingizwa kutoka nje kwa
mwaka. Utafiti umeonesha kwamba Tanzania inaweza kuzalisha kiwango cha
kutosheleza mahitaji ya nchi iwapo kutakuwa na kilimo cha umwagiliaji, miche
bora ya miwa, pembejeo za kilimo zilizo bora ikiwemo mbolea pamoja na mazingira
bora ya uwezeshaji (enabling environment) wa sekta ya sukari.
|
Maofisa wa NMB
Idara ya biashara ya Kilimo, kwanza kulia ni Sierk Plaat ambae ni
Mchambuzi Mwandamizi toka benki ya Rabobank, Robert Paschal Mkuu wa Idara
Mikopo ya Kilimo NMB na Carol Nyangaro Mtafiti, Mchambuzi wa mambo ya
kilimo wakionyesha kitabu ambacho kimebeba ripoti ya mfumo wa stakabadhi
ghalani |
Mkuu
wa Idara ya biashara za kilimo NMB, Robert Paschal (kati) akiongea na
waandishi wa habari na kuwasilisha ripoti ya biashara za kilimo zifanywazo na
Benki ya NMB
Sehemu ya
waandishi wa habari waliohudhuria hafla ya uwasilishaji wa ripoti ya
biashara ya kilimo
Sehemu ya maofisa wa NMB wanaoshiriki Maonesho ya Biashara yanayoendelea
Comments