NMB YAWEZESHA MKUTANO WA WASAMBAZAJI MAFUTA NA GESI NCHINI TANZANIA

Mwishoni mwa wiki NMB ilifadhili mkutano wa makampuni na taasisi ambazo wamepewa dhamana ya uchimbaji na usambazaji wa mafuta na gesi nchini. Mkutano huo ulifanyika katika hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam kwa siku mbili ukiambatana na maonyesho ya biashara kutoka makampuni tofauti nchini Tanzania.

Dhumuni kubwa la mkutano huu lilikuwa ni kutengeneza mahusiano baina ya  wafanya biashara na kujadili jinsi ambavyo huduma zitolewazo  na makampuni na taasisi zilizopewa dhamana ya uchimbaji na usambazaji wa mafuta na gesi nchini  zinavyoweza kuisaidia jamii husika.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Miamala kwa Taasisi NMB, Gerald Kamugisha akielezea jinsi NMB inavyoweza kusaidia makampuni na taasisi mbali mbali zinazosambaza mafuta na gesi nchini Tanzania.
 Kamishina wa Nishati na masuala ya Petroli, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Hosea Mbise,akimkabidhi cheti Mkuu wa kitengo cha huduma za miamala kwa taasisi NMB, Gerald kamugisha kwa udhamini ambao NMB umetoa ili kufanikisha mkutano huo.
 Meneja ukuzaji wa biashara NMB, Masato Wasira akiwaelezea baadhi ya washiriki wa mkutano huo juu ya huduma zitolewazo na benki ya NMB.
Sehemu ya washiriki wa mkutano wakisikiliza kwa makini.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.