Pembe haramu kutoka UG zanaswa Kenya


Bara la Asia lina soko kubwa sana la pembe za Ndovu
Pembe haramu za ndovu zilizokuwa zinasafirishwa kutoka Uganda hadi Malaysia, zimenaswa katika bandari ya Mombasa pwani ya Kenya.
Pembe hizo zilikuwa zimefunikwa kiasi cha kufanana na samaki waliokaushwa.
Mzigo huo wa takriban pembe 770 kutoka nchi Uganda, ulikuwa unapelekwa Malaysia.
Walanguzi hao pia walikuwa wamebeba samaki waliokuwa na harufu mbaya ambayo huwachukiza Mbwa maalum wa uchunguzi, kulingana na msemaji wa shirika la ulinzi wa wanyapori nchini Kenya Paul Udoto.
Pembe za Ndovu zina soko kubwa sana barani Asia, ambazo hutumiwa kwa vitu vya urembo.
Serikali ya Kenya iliharamisha biashara za pembe za ndovu mwaka 1989, huku viwango vya uwindaji haramu wa Ndovu vikipungua pakubwa, lakini pameanza kuonekana ongezeko la uwindaji haramu tena wa Ndovu katika miaka ya hivi karibuni.
Bwana Udoto alisema stakabadhi kuhusu pembe hizo zilolionyesha kuwa zilisafirishwa kutoka Uganda kwa gari tarehe 12 mwezi Juni.
Gari hilo kisha likaegeshwa katika kituo cha mafuta mjini Mombasa, eneo la kufanyia biashara hadi mzigo huo ulipofikishwa bandarini.
Thamani ya pembe hizo badi haijabainika kwa mujibu wa bwana Udoto.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI