Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akikagua guard ya wahitimu wa Jeshi la Polisi na Uhamiaji kabla ya kuyafunga mafunzo ya wahitimu hao ya awali yaliyofanyika katika Chuo Cha Polisi (CCP) mjini Moshi jana .Wahitimu 3,092 wakiwemo askari wa Uhamiaji 51 walimaliza mafunzo hayo jana. Dk. Nchimbi katika hotuba yake aliwataka wahitimu hao kufanya kazi kwa uadilifu katika vituo mbalimbali vya kazi watakavyopangiwa nchini.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil pamoja na viongozi mbalimbali wa wizara na maofisa wa Jeshi la Polisi wakati alipokuwa anawasili katika viwanja vya Chuo Cha Polisi (CCP), mjini Moshi kwa ajili ya kufunga mafunzo ya awali ya Polisi na Uhamiaji. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akifungua bomba la maji la kisima baada ya kukizindua katika Chuo Cha Polisi (CCP) mjini Moshi. Dk Nchimbi pia alitembelea miradi mbalimbali iliyopo ndani ya chuo hicho kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya Polisi na Uhamiaji namba 1/2012/2013.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kulia) akimkabidhi zawadi mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri katika masomo yao wakati wa mafunzo ya awali ya Polisi na Uhamiaji yaliyofanyika katika Chuo Cha Polisi (CCP) mjini Moshi leo. Wahitimu 3,092 wakiwemo askari wa Uhamiaji 51 walimaliza mafunzo hayo Jana. Dk. Nchimbi katika hotuba yake aliwataka wahitimu hao kufanya kazi kwa uadilifu katika vituo mbalimbali vya kazi watakavyopangiwa nchini.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akitoa hotuba yake kwa wahitimu wa mafunzo ya awali ya Polisi na Uhamiaji (hawapo pichani) kabla ya kuyafunga mafunzo hayo katika Uwanja wa Chuo Cha Polisi (CCP) mjini Moshi. Wahitimu 3,092 wakiwemo askari wa Uhamiaji 51 walimaliza mafunzo hayo jana. Dk. Nchimbi katika hotuba yake aliwataka wahitimu hao kufanya kazi kwa uadilifu katika vituo mbalimbali vya kazi watakavyopangiwa nchini.


PICHA ZOTE NA FELIX MWAGARA  
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*