TAASISI YA STARKEY FOUNDATION YASAIDIA WATU 3500 WENYE ULEMAVU WA KUSIKIA

 Muasisi wa Taasisi ya Strakey Hearing Foundation,  Bill Starkey akimhudumia mtoto Lissa Frank (9) ambaye alikuwa kiziwi tangu kuzaliwa na kuweza kusikia baada ya kupata tiba na huduma ya kuwekewa kifaa maalumu katika kliniki maalumu iliyofanyika katika Hospitali ya Seliani, mkoani Arusha
Nyota wa mchezo wa mpira wa miguu wa Marekani (American Football) Rays Lewis akimpa  Rais  Jakaya Kikwete zawadi ya kofia yenye nembo ya timu yake wakati nyota huyo alipomtembelea Rais Kikwete mjini Arusha jana. Nyota huyo yuko nchini ambapo ni mmoja wa wafadhili wakubwa wa huduma kwa wagonjwa wenye ulemavu wa kusikia inayotolewa na Taasisi ya Starkey Hearing Foundation ya nchini Marekani.Wagonjwa zaidi ya 3500 wanatarajiwa kunufaika na huduma hiyo inayotolewa bure na taasisi hiyo. (PICHA NA FREDDY MARO)

WALEMAVU WA KUSIKIA WANUFAIKA NA HUDUMA ILIYOTOLEWA NA TAASISI YA STARKEY HEARING FOUNDATION.
Na.Freddy Maro,Seliani Arusha.
Julai, 7 ,2013
Zaidi ya Watanzania 3500 wenye maradhi ya kusikia wanatarajiwa kunufaika kwa huduma ya tiba inayotolewa na Taasisi ya Starkey Hearing Foundation yenye makao yake jijini Washington nchini Marekani.
Muasisi wa Taasisi ya Starkey Hearing foundation  Bwana Bill Austin  Starkey ameyasema hayo wakati wa kliniki maalumu ya kuwatibu watu wenye maradhi mbalimbali ya kusikia iliyokuwa ikifanyika Katika hospitali ya Seliani mjini Arusha baada ya kutoa huduma hiyo katika miji ya Dar es Salaam na Moshi mkoani Kilimanjaro.
“Nimefurahishwa sana na kutiwa moyo kwa kazi tuliyoifanya ya kuwahudumia watu na kuwawezesha kusikia ambapo wengine ndiyo wameweza kusikia kwa mara ya kwanza tangu walipozaliwa.Furaha yao ni kitu cha kutia moyo sana katika juhudi zetu.Madaktari wa kitanzania tulioshirikiana nao wamefanya kazi kubwa na nzuri” alisema Bwana Starkey ambaye ameambatana na timu ya wataalamu na watu mashuhuri kutoka nchini Marekani ambao wametoa misaada mbalimbali kugharamia kampeni hiyo.

Bwana Starkey amesema kuwa watu wengi walijitokeza wakati wa kliniki hiyo maalumu kwa watu wenye ulemavu wa kusikia na kuongeza kuwa katika siku tatu walizokuwa mjini Arusha wagonjwa zaidi ya 600 walipatiwa huduma hiyo ya matibabu  kwa kuwekewa vifaa maalumu katika masikio yako na kuwawezesha kusikia vyema na kusema kila mwaka shirika lake litafanya mipango ya kuhakikisha kwamba huduma hiyo inakuwa endelevu.

Mwandishi wa habari hizi alishuhudia wazazi wenye furaha baada ya kuona watoto wao wenye umri kati ya miaka mitano na kumi wakiweza kusikia vyema kwa mara ya kwanza katika maisha yao  baada ya kupatiwa matibabu kwa kuwekewa vifaa maalumu katika masikio yao huduma ambayo imetolewa bure na shirika hilo na isingekuwa rahisi kuipata kwa watu wengi walio na kipato cha chini.

Bwana Bill Austin Starkey aliwashukuru wafadhili mbalimbali waliowezesha mpango huo wa matibabu kufanikiwa  na kuongeza kuwa falsafa ya taasisi yake ni “Ili Dunia ipate kusikia” imeweza kutekelezwa kwa vitendo kwa sababu  anaamini kuwa kukiwa na nia ya dhat na moyo wa kushirikiana kutekeleza jambo fulani mafanikio ni bayana na mabadiliko mengi chanya yatawezekana katika ulimwengu.

Bill Austin Starkey  na mkewe Tani Austin ambaye ni muasisi mwenza wa taasisi hiyo pamoja na washirika wao wanatarajia kwenda nchini Malawi kutoa huduma kama hiyo na baadaye kurejea tena nchini kutoa huduma  kabla ya kuondoka kurejea nchini marekani.

Mmoja wa wataalamu wanaotoa huduma katika kliniki hiyoDkt. Ron Brouillete alisema mbali na kuzaliwa na ulemavu wa kutosikia wangojwa wengine waliotibiwa katika kliniki hiyo walipata madhara ya kutosikia kutokana na matumizi holela ya dawa ya kutibu Malaria aina ya Quinine.

“Napenda kutoa ushauri kwa madaktari na wahudumu katika sekta ya afya kuepuka kuwapa dawa ya Quinine wagonjwa wa Malaria.Dawa hii itumike kwa uangalifu mkubwa na pale ambapo dawa nyingine zimeshindwa kumtibu Mgonjwa,” alisisitiza mtaalamu huyo kutoka nchini Marekani .


Mmoja wa wafadhili wa mradi huo anayefuatana na Bwana Bill Austin Starkey ni mcheza mpira  wa miguu maarufu wa Marekani(American Professional Football) Bwana Ray Lewis ambaye pia anachezea ligi ya taifa ya mpira wa miguu ya nchi hiyo(National Football League).


Awali Mchezaji huyo alimtembelea Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete aliyekuwa mapumzikoni mjini Arusha na kusema kuwa Rais Kikwete ni mmoja kati ya viongozi mashuhuri barani Afrika wenye maono ya mbali na nia ya dhati ya kuwahudumia wananchi wake.

“Nimesoma habari nyingi mambo mangi yenye mafanikio makubwa anayoyafanya Rais Kikwete na nilipopata fursa ya kuja nchini Tanzania nikatumia nafasi hiyo kuja kumsalimia,kumsikiliza na kumpongeza.Ni mtu mnyenyekevu sana na nimefurahi sana kumtembelea na kuongea naye,” alisema nyota huyo wa mpira wa miguu Marekani muda mfupi baada ya kukutana na Rais Kikwete ambapo alimzawadia kofia yenye nembo ya timu yake.

Bill Austin Starkey na mkewe Tani Austin waliunda Taasisi ya Starkey Hearing foundation mwaka 1984 kwa lengo la kusaidia watu wenye maradhi ya kusikia na mpaka sasa maelfu ya watu katika sehemu mbalimbali duniani wamenufaika na huduma inayotolewa na taasisi hiyo.
Mwisho

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.