TIGO KUWANUFAISHA WATEJA WAO KWA KUWAZAWADIA BAJAJI 60 KUPITIA PROMOSHENI MPYA YA 'MILIKI BIASHARA YAKO'
Meneja Mkuu Uendeshaji wa Kampuni inayouza Bajaj ya Fair Deal Auto (PVT) Limited, Anil Dewan (kulia) akimkabidhi Meneja wa Chapa ya Tigo, William Mpinga moja kati ya Bajaj 60 zitakazotolewa zawadi kwa washindi wa promosheni mpya ya 'Miliki Biashara Yako'inayolenga kuwainua wateja wo kiuchumi. Hafla hiyo imefanyika Dar es Salaam leo
Mpinga akikabidhiwa ufunguo
Mpinga akiwa ndani ya Bajaj
Wakiwa na furaha baada ya makabidhiano
Tigo
kuwezesha wateja wake kiuchumi kupitia promosheni ya Miliki Biashara Yako
Dar es
Salaam, Julai 18, 2013 – Tigo Tanzania
leo imezindua promosheni kabambe iitwayo “Miliki Biashara Yako” inayolenga
kuwainua wateja wake kiuchumi kwa kuwapatia fursa ya kushinda usafiri wa Bajaji
60 kwa muda wa miezi miwili ambapo kila siku mteja atajishindia Bajaji moja.
Akitangaza promosheni hiyo katika mkutano na wanahabari,
Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga alisema, “Tigo inatambua jukumu lake tulionao
katika kuboresha maisha ya Watanzania, na kwa sababu hiyo tumeamua kuzindua
promosheni ya aina hii kwa ajili ya kugusa zaidi maisha ya watu. Kwa mara
nyingine tena tunawapa wateja wetu sababu ya kutabasamu wakiwa na Tigo kwa
kuwapatia nafasi ya kumiliki biashara yao wenyewe kupitia promosheni hii ya “Miliki
Biashara Yako”. Hii ni nafasi yakipekee ambapo wateja wetu watapata fursa ya kuwa
wajasiriliamali, kujipatia kipato, kutoa ajira, pamoja na kutoa huduma ya
usafiri wenye gharama nafuu kwa jamii.”
Wateja wa Tigo wanaweza kujishindia Bajaji moja kila siku
kwa muda wa siku 60 kwa kuongeza vocha ya Tsh 1,000 tu kwa siku. Ili kuhakikisha
kuwa wateja wengi wanafurahia promosheni hii, mteja hahitaji kuweka vocha ya
Tsh 1000 kwa mkupuo mmoja ili kushiriki, anaweza kuongeza salio kidogo kidogo
hadi kufikisha kiasi cha Tsh 1000 kwa siku na kuweza kuingia kwenye droo. Vile
vile mteja anaweza kuongeza salio mara nyingi awezavyo ili kujiongezea nafasi zaidi
ya kujishindia Bajaji. Pamoja na hayo, ili kuwapatia urahisi zaidi wateja, bado
mteja anaruhusiwa kuongeza salio pitia namna zote zile ikiwemo Tigo Rusha, Tigo
Pesa au kwa vocha ya kawaida.
“Tunaamini kwamba promosheni hii itawapatia wateja wetu
sababu nyingine yakutabasamu. Wateja 60 watakaopatikana washindi watajinyakulia
Bajaji mpya kabisa ambapo wataweza kuzitumia kuanzisha biashara zao wenyewe.
Biashara ya Bajaji ni biashara yenye faida sana, kwa siku mmiliki wa Bajaji
anaweza kuingiza kipato cha kati ya Tsh 25,000 mpaka Tsh 30,000 kwa siku, sawa
na Tsh 900,000 kwa mwezi, ambayo ni Tsh 10,800,000 kwa mwaka,” alielezea
Mpinga.
Bw. Mpinga alisema kwamba kila Bajaji ina thamani ya Tsh 6,700,000.
“Tayari Tigo imechukua jukumu la kulipia leseni ya barabara (road license) na
bima ya Bajaji. Kwahiyo mteja atakuwa amebakiwa na jukumu la kuja kuchukua
Bajaji yake na kuanzisha biashara yake mara moja,” alimalizia Mpinga.
KUHUSU TIGO:
Tigo ni mtandao wa kwanza wa simu
za mkononi nchini Tanzania. Ilianza shughuli mwaka 1994 na inapatikana katika mikoa
ishirini na sita (26)
Tanzania bara na visiwani.
Lengo la Tigo ni kuwa mtandao
unaoongoza kwa kutoa huduma bora na za ubunifu Tanzania kwa wateja wake wote
ambazo zinaendana na mahitaji yao kuanzia huduma za sauti za bei nafuu,
vifurushi vya intaneti vyenye kasi kubwa na huduma bora za fedha za simu za
mkononi kupitia Tigo Pesa.
International Cellular S.A (MIC)
ambayo ni ya unafuu wa huduma na inapatikana kirahisi kwa zaidi ya wateja milioni 43 katika masoko
13 barani
Afrika na Amerika ya Kusini.
"Tabasamu
upo na Tigo"
Kwa
maelezo zaidi wasiliana na:
Amani Nkurlu – Meneja Mahusiano
+255 658 870 107 au +255 712 223 839
Comments