Meneja Bidhaa wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo, Husn Seif (kushoto) akibofya kwenye kompyuta kumpata mmoja wa wateja watatu walioshinda Bajaji katika droo ya kwanza ya Promosheni ya 'Miliki Biashara Yako' iliyofanyika mchana huu jijini Dar es Salaam. Walioshinda ni Mohamed Ramadhan, Adam Said Kalulu na Riziki Lucas Kisema wote wakazi wa Dar es Salaam.Anayeshuhudia ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya Kusimamia Michezo ya Kubahatisha, Chiku Saleh.
Promosheni hiyo iliyoanza Ijumaa iliyopita itawanufaisha wateja 60 kwa kila mmoja kuzawadiwa Bajaji moja. Kiingilio ni kuweka kwenye simu salio kuanzia sh. 1000 kwa siku. Hafla ya kuwakabidhi bajaji washindi hao itafanyika Alhamis ijayo jijini Dar es Salaam (PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Meneja Chapa ya Tigo, William Mpinga akiwasiliana kwa simu na mmoja kati ya wateja watatu walioshinda promosheni hiyo.
Promosheni hiyo iliyoanza Ijumaa iliyopita itawanufaisha wateja 60 kwa kila mmoja kuzawadiwa Bajaji moja. Kiingilio ni kuweka kwenye simu salio kuanzia sh. 1000 kwa siku. Hafla ya kuwakabidhi bajaji washindi hao itafanyika Alhamis ijayo jijini Dar es Salaam (PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Meneja Chapa ya Tigo, William Mpinga akiwasiliana kwa simu na mmoja kati ya wateja watatu walioshinda promosheni hiyo.
Comments