Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa
Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna mara alipowasili katika Uwanja wa
ndege wa Kimataifa wa Muscat kuanza Ziara ya kikazi nchini Oman, kushoto
ni Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman Mhe. Dr. Rawiyah Al Busaidi, wa
kwanza kulia ni Mheshimiwa Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini
Oman.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa
Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna wa pili kutoka kushoto akiwa
katika mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman Mhe. Dr. Rawiyah Al
Busaidi, wa pili kulia , wa kwanza kushoto ni Mheshimiwa Ali Ahmed
Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa
Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna wa tatu kulia akiongoza ujumbe wa
Zanzibar katika mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman Mhe. Dr.
Rawiyah Al Busaidi akiongoza ujumbe wa Oman Kushoto , wa nne kushoto ni
Mheshimiwa Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa
Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna kushoto na Waziri wa Elimu ya Juu
wa Oman Mhe. Dr. Rawiyah Al Busaidi wakitia saini nyongeza katika
mkataba wa ushirikiano wa Elimu ya Juu baina ya Oman na Zanzibar.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa
Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna kushoto akiwa katika Mazungumzo na
Waziri Kazi wa Oman kuhusu ushirikiano katika sekta ya mafunzo ya
amali.
Comments