Rapa kinda wa Nigeria anayekuja kwa kasi kama treni ya umeme,
hapa namzungumzia Davido, ameonekana akiwa kwenye studio za Rapa wa
marekani mwenye asili ya Nigeria ‘Wale’ anayefanya kazi chini ya lebo ya
Maybach Music Group inayomilikiwa na Rick Ross .
Wakiwa studio, mastaa hao waliweza kupiga pamoja picha na kisha kuzitupia mtandaoni. “Chilling at my spot wit @lifeofdavido writin these naija tunes” aliandika Wale kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Bado haijaweza kufahamika kama wawili hao wapo kwenye
mchakato wa kufanya nyimbo pamoja au la, licha ya dalili kujionyesha.
Endelea kutembelea blog hii kuhusiana na taarifa zaidi.
Comments