Wachezaji wa Liverpool, Steven Gerrard akimpongeza Martin Skrtel.
Liverpool imeifunga bao 3 – 2 vijana wa Manchester City
katika mchezo uliochezwa katika dimba la Anifield. Mabao ya Liverpool
yakifungwa na mchezaji Raheem SterLing, Martin Skrtel na Phillippe
Coutinho huku kwa upande wa City wafungaji wakiwa ni David Silva na moja la kujifunga kutoka kwa Glen Johnson.
Mchezo mwingione ukipigwa kule kwa Swansea City wakiwaalika
watoto wa Jose Mourinho Chelsea ‘The Blues’ . Chelsea iliibuka na
ushindi wa bao moja kwa bila, bao lililofungwa ba Demba Ba mnamo
dakika ya 68 na hivyo kuwapa ushindi gharabu ugenini.
Hivi ndicho alichofanya Demba Ba wa Chelsea baada ya kufunga.
Msimamo wa ligi hivi sasa mara baada ya mchezo wa leo
inawafanya LiverPool wasalie kileleni wakiwa na Pointi 77 wakicheza
michezo 34 ikisalia michezo 4 mkononi kumaliza ligi hiyo.
Chelsea wanashikilia nafasi ya pili wakiwa na Pointi 75 ikiwa
ni tofauti ya pointi na Liverpool, wote wakicheza michezo 34 huku
ikisalia minne.
Manchester City baada ya kunyukwa hii leo, wanasalia nafasi
tatu wakiwa na Pointi 70, tofauti ya pointi saba na Liverpool, na
tofauti ya Pointi tano na Chelsea huku wakiwa wamebakiwa na michezo
miwili kumaliza ligi.
Evertoon mara baada ya kupata ushindi hapo jana, imejikita
nafasi ya nne ikiwa na pointi 66 ikiwa tayari imeshacheza michezo 33
ikisalia michezo mitano mkononi.
Tazama Video za magoli hapo chini
Comments