LIVERPOOL WASALIA KILELENI, WAICHAPA 3-2 MAN CITY, CHELSEA YAIKALISHA SWANSEA KIMOJA.

Gerrard akimuhug Martin Skrtel
Wachezaji wa Liverpool, Steven Gerrard akimpongeza Martin Skrtel.
Liverpool imeifunga bao 3 – 2 vijana wa Manchester City katika mchezo uliochezwa katika dimba la Anifield. Mabao ya  Liverpool yakifungwa na mchezaji Raheem SterLing, Martin Skrtel na Phillippe Coutinho huku kwa upande wa City wafungaji wakiwa ni David Silva na moja la kujifunga kutoka kwa  Glen Johnson.
Mchezo mwingione ukipigwa kule kwa Swansea City wakiwaalika watoto wa Jose Mourinho Chelsea ‘The Blues’ . Chelsea iliibuka na ushindi wa bao moja kwa bila, bao lililofungwa ba  Demba Ba  mnamo dakika ya 68 na hivyo kuwapa ushindi gharabu ugenini.
Demba Ba
Hivi ndicho alichofanya Demba Ba wa Chelsea baada ya kufunga.
Msimamo wa ligi hivi sasa mara baada ya mchezo wa leo inawafanya LiverPool wasalie kileleni wakiwa na Pointi 77 wakicheza michezo 34 ikisalia michezo 4 mkononi kumaliza ligi hiyo.
Msimamo wa ligi ya Uingereza.
Chelsea wanashikilia nafasi ya pili wakiwa na Pointi 75 ikiwa ni tofauti ya pointi na Liverpool, wote wakicheza michezo 34 huku ikisalia minne.
Manchester City baada ya kunyukwa hii leo,  wanasalia nafasi tatu wakiwa na Pointi 70, tofauti ya pointi saba na Liverpool, na tofauti ya Pointi tano na Chelsea huku wakiwa wamebakiwa na michezo miwili kumaliza ligi.
Evertoon mara baada ya kupata ushindi hapo jana, imejikita nafasi ya nne ikiwa na pointi 66 ikiwa tayari imeshacheza michezo 33 ikisalia michezo mitano mkononi.
Tazama Video za magoli hapo chini

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.