MASHINDANO YA TANZANIA MOVIE TALENTS KUHAMIA KANDA YA KATI MKOANI DODOMA, ZOEZI LA KUTAFUTA WASHINDI KUANZA JUMAMOSI YA WIKI HII
Na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mwanza
Hatimaye
Kikosi Kazi cha Kampuni ya Proin Promotions Limited ambao ndio waratibu
na waandaaji wa Mashindano ya Kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania
yajulikanayo kama Tanzania Movie Talents (TMT) kinaondoka leo asubuhi
Mkoani Mwanza Kuelekea Mkoani Dodoma kwaajili ya kuendelea na shindano
la kusaka vipaji vya kuigiza katika Kanda ya Kati.
Ambapo mashindano yatafanyika Mkoani Dodoma katika Ukumbi wa African Dream kuanzia Jumamosi ya tarehe 12 April 2014 kuanzia Saa moja asubuhi hadi tarehe 15 April 2014, kabla ya mashindano hayo kufanyika Mkoani Dodoma mnamo Siku ya Ijumaa tarehe 11 April 2014 kutakuwa na Promo pati itakayofanyika katika Ukumbi wa Disco wa 84 Mjini Dodoma na Wasanii Lulu, Joti, Rich Rich, Monalisa na MC Pilipili watakuwepo ndani ya nyumba.
Ambapo mashindano yatafanyika Mkoani Dodoma katika Ukumbi wa African Dream kuanzia Jumamosi ya tarehe 12 April 2014 kuanzia Saa moja asubuhi hadi tarehe 15 April 2014, kabla ya mashindano hayo kufanyika Mkoani Dodoma mnamo Siku ya Ijumaa tarehe 11 April 2014 kutakuwa na Promo pati itakayofanyika katika Ukumbi wa Disco wa 84 Mjini Dodoma na Wasanii Lulu, Joti, Rich Rich, Monalisa na MC Pilipili watakuwepo ndani ya nyumba.
Mashindano
haya yatakuwa ni muendelezo wa mshindano yaliyoanza kufanyika katika
Kanda ya ziwa Mkoani Mwanza ambapo Washindi watatu kutoka Mkoani Mwanza
wakiwakilisha Kanda ya Ziwa wakiwa wameshapatikana na kila mshindi
aliweza kupewa zawadi ya shilingi laki tano kila mmoja na kusubiria
kwenda Mkoani Dar Es Salaam kwaajili ya kuungana na washindi wengine Wa
kanda zilizobaki kwaajili ya Fainali kubwa itakayofanyika mkoani Dar Es
Salaam
Comments