498 Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA toka Ofisi
ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Emmanuel
Mahinga akitoa maelezo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam (hawapo
pichani) kuhusu jinsi Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma (EPICOR 9.05)
unavyofanya kazi na malengo ya kuanzishwa kwa mfumo huo ikiwemo
kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo hapa nchini. Picha zote
na Frank Mvungi -Maelezo.
Afisa
Msimamizi wa Fedha (TEHAMA) toka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Elisa
Rwamiago (katikati)akifafanua kwa waaandishi wa habari jinsi Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma (EPICOR
9.) utakavyoongeza tija katika utendaji wa Serikali za Mitaa na kuondoa
malalamiko ya kuwepo mianya ya vitendo
vya ubadhilifu wa fedha za umma.kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Serikalini toka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Bi Rebecca Kwandu.kulia, ni
Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bi Georgina Misama.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka
Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bi Rebecca
Kwandu (kushoto) akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar
es salaam kuhusu faida za matumizi ya Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma
(EPICOR 9.05) Katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo Halmashauri 133 na
Mkoa 21 ya Tanzania Bara imeunganishawa katika mfumo huo, katikatika ni Afisa
Msimamizi wa Fedha (TEHAMA) toka
TAMISEMI Bw. Elisa Rwamiago na kulia ni
Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bi Georgina Misama.
Comments