Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bwn. Suleiman Saleh akifuatilia kikao.
Mwenyekiti
wa kamati ya Vijimambo Bwn. Baraka Daudi akitia saini kitabu cha wageni
Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani siku kamati ilipokutana na Ubalozi
kwa kikao cha Maandalizi ya sherehe ya miaka 4 ya Vijimambo ambayo
mwaka huu mbiu yake ni kutangaza Utalii na kukemea ujangili kwa nguvu
zote karibu tuungane pamoja katika siku hii maalumu ili wewe, mimi
pamoja na yule wakiwemo watoto wetu wajifunze mengi kuhusu Utalii wa
nchi yetu ukiwemo kukemea nguvu zote swala zima la ujangili mali asili
za nchi yetu.
Kaimu
Katibu wa kamati ya Vijimambo Bwn Julius Katanga akitia saini kitabu
cha wageni Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani siku kamati ya maandalizi
ilipokutana na Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kwa ajili ya
maandalizi ya sherehe ya miaka 4 ya Vijimambo itakayofanyika September
13, 2014.
Balozi
wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akiongoza kikao siku
kamati ya maandalizi ya sherehe ya miaka 4 ya Vijimambo ilipokutana na
Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kwa ajili ya maatayarisho ya mwanzo
mwanzo ya sherehe hizo.
Comments