Msama Promotions yatangaza Viingilio Tamasha la Pasaka

Sehemu ya Umati wa watu uliohudhuria tamasha la pasaka mwaka jana katika uwanja wa Taifa.

KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, mwishoni mwa wiki iliyopita ilitangaza viingilio vya tamasha hilo litakalofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, viti vya kawaida ni shilingi 5000 na watoto 2000.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Alex Msama viti maalum ni shilingi 20,000 wakati VIP  ni shilingi 10,000.Msama alisema hivi sasa wanaendelea na mchakato wa kufanikisha zoezi la mgeni rasmi katika tamasha hilo kwani hivi karibuni watakamilisha zoezi la upigaji kura kumchagua. Msama alisema mchakato wa kuelekea katika tamasha hilo litakalofanyika jijini Dar es Salaam Aprili 20 na baadaye mikoa mingine saba hapa nchini.

Aidha Msama alitoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam kujiandaa na tamasha hilo ipasavyo kwani lina mlengo wa kurudisha mapato yanayopatikana na kuyapeleka katika maeneo matatu ambayo yanawahusu, yatima, walemavu na wajane.

Msama alisema mipangilio yake ya kuwawezesha wenye uhitaji maalum ni kuwajengea kituo kitakachokuwa katika eneo la Pugu nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam ambacho kitajulikana kama Jakaya Mrisho Kikwete, rafiki wa wasiojiweza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU