Nchimbi mgeni rasmi Tamasha la Pasaka Songea.

 
ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi anatarajia kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Aprili 26 Wilayani Songea mkoani Ruvuma.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama wakazi wa mkoa huo na maeneo ya jirani wajitokeze kwa wingi  kufanikisha sherehe ya kufufuka kwa mwokozi Wetu Yesu Kristo.
 Msama alisema mbali ya Nchimbi kuwa mgeni rasmi Songea, jijini Mbeya mgeni rasmi atakuwa ni Mbunge wa viti maalum, Mary Mwanjelwa  wakati mkoani Dodoma mgeni rasmi atakuwa mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwine. Aidha Msama alitoa fursa kwa wakazi wa mikoa litakapofanyika Tamasha la Pasaka kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha ufanikishaji wa ujenzi wa Kituo cha Kimataifa cha wenye uhitaji Maalum cha Jakaya Mrisho Kikwete rafiki wa Wasiojiweza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*