NITETEE FOUNDATION YAZINDULIWA RASMI JIJINI MWANZA KUTETEA WANAWAKE NA WATOTO WANAOSHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU TANZANIA.

 Mtoto Veronica ambae ni mmoja ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu walioibuliwa na taasisi ya Nitetee akitoa ushuhuda wa maisha yake yeye na wadogo zake baada ya baba yao kufungwa jela kwa kesi ya mauaji na kasha mama yao kuwakimbia na kwenda kwa mwanaume mwengine. Kwa mujibu wa Veronica anasema baba yao amefungwa kwa kusingiziwa kwani siku mauaji hayo yakitokea baba yake alikuwa ndani anaumwa, na tukio hilo limezima ndoto zote za maisha yake na wadogo zake.
 1.   Meya wa Jiji la Mwanza Mh. Stanislaus Mabula (kushoto) akizungumza na wageni waalikwa (hawapo pichani) na kumpongeza Mkurugenzi wa Nitetee Foundation kwa moyo wake wa kujitoa katika kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum. Mh meya aliahidi kufanya kazi na taasisi hiyo katika lengo la kutetea watu wengi Zaidi ambae nae alichangia magodoro sita. Katikati ni Mshehereshaji wa hafla hiyo ambae ni Mtangazaji wa kituo cha Start TV Bi. Ivona Kamonte na msanii H-Baba.
 Baadhi ya misaada iliyoletwa na wageni waalikwa katika kusaidia familia zaidi ya 25 zilizo katika mazingira magumu chini ya taasisi ya Nitetee.
  Kina mama wa jiji la Mwanza walihudhuria hafla ya uzinduzi wa jiji la Nitetee Foundation katika Hoteli ya New Mwanza.

1.   Mama Tizeba (kulia), Mke wa Naibu Waziri wa Uchukuzi ambae alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa taasisi ya Nitetee wakifungua kwa pamoja pazia na Bi Flora Lauwo (kushoto), Mkurugenzi na Muasisi wa Nitetee Foundation kuashiria uzindizu rasmi wa taasisi hiyo katika hafla iliyofajiaka Jumapili Jioni katika Ukumbi wa New Mwanza Hotel, jijini Mwanza.

Nguvu imeongezeka katika jitihada za kusaidia jamii ya wanaoishi mazingira magumu hapa nchini baada ya kuzinduliwa taasisi inayojishughulisha na kutoa misaada ya kibinaadamu kwa wanawake na watoto walio kwenye mahitaji makubwa hasa jamii ya vijijini na nje ya miji, inayojulikana kama NITETEE FOUNDATION toka jijini Mwanza. 
 Shirika hilo la maendeleo kwa ajili ya wanawake na watoto nchini Tanzania lilizinduliwa usiku wa Jumapili na mgeni rasmi ambae alikuwa ni mke wa Naibu Waziri wa Uchukuzi Mama Charles Tizeba katika ukumbi wa New Mwanza Hotel, iliyopo jijini Mwanza. 
Tukio hilo la aina yake lilipendezeshwa na wenyeji wa mkoa wa Mwanza pamoja na watu maarufu kadhaa, viongozi wa vyama na jiji la Mwanza akiwemo Stanislaus Mabula, Mwanamuziki Stara Thomas na H-Baba, Katibu CCM mkoa wa Mwanza Bi Joyce Masunga. 
Akiongea na wageni walihudhuria katika uzinduzi huo Mgeni rasmi ambae ni Mke wa Waziri wa Uchukuzi Mama Charles Tizeba aliwasihi wanawake nchini kutunza familia zao na kutowaacha wakaitwa watoto wa mitaani. 
 “Wimbi hili la watoto mpaka hii leo hata wengine kufikia hatua ya kuwaita watoto wa mtaa kana kwamba wanazaliwa na mitaa tuna uwezo wa kuliondoa endapo tu, wakina mama tutasimamia kwanza misingi ya walezi, ama wazee wetu kwa kurudisha dhana ya ‘MTOTO WA MWENZIO NI WAKO PIA” alisema mama Tizeba na kuhoji “haya maneno ya sugar mamy, sugar dady, sijui vidumu, wamama haya maneno yanatoka wapi?”
 Akizungumza wakati wa uzinduzi huo muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa NITETEE Foundation Bi. Flora Lauwo amesema kwamba Taasisi ya NITETEE imekuwa ikifanya shughuli zake za kuwasaidia watoto kutoka familia zenye kipato cha chini vijijini na pembezoni mwa mji ili waweze kupata fursa ya kupata elimu pamoja na wanawake kupata fursa za kujikwamua kiuchumi. “Malengo yetu ni kutoa na kuongeza kasi ya maendeleo hapa nchini hasa katika sekta ya elimu. 

Hivyo basi miradi yetu italenga kuhamasisha jamii ya kipato cha chini ambao hawawezi kuwapatia elimu watoto wao hasa maeneo ya vijijini na pembezeno mwa miji na kupunduzo matatizo ya moja kwa moja kwa jamii hizi pamoja na matatizo ya saikolojia wanazokumbana nazo watoto, vijana pamoja na wanawake” alisema Mkurugenzi wa Nitetee Bi. Flora .
 “Lengo la Ntetee ni kufikia jamii zote za Tanzania nzima, kwa kuanza tumeanza moja kwa moja kwenye ngazi ya familia ambapo tunamgusa mototo na mama ama mlezi ambaye anasimamia kuleta ustawi wa mtoto huyu, tutahangaika kwanza kubaini hizo familia zenye kusongwa na uduni wa maisha usio na msaada, baada ya kujiridhisha tutaambatana na familia hizo kushirikisha watanzania wengine kuona uhitaji huo ili kuweza kusaidia kwa namna Mungu anavyotuwezesha watu wake.” aliongeza Bi. Flora.

 Bi Flora alimalizia kwa kusema kwamba “Kwa kuanzia taasisi hii mpaka sasa tumetembelea familia 25 zote za kutoka hapa jijini mwanza, kati ya hizo familia baada ya kuridhia, tumejitahidi kadri ya uwezo wetu kutoa msaada ambao tulishirikiana na marafiki wachache tuliokuwa tukizungumza nao juu ya hizo familia na kutoa mahitaji muhimu naya karibu kwa kadri tulivyoweza kwa baadhi tu ya hizo familia” .

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.