Mganga
Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala Dkt. Kariamel Wandi(kushoto)
akimshukuru Meneja wa NMB kanda ya Dar es salam Bw. Salie Mlay kwa
kumkabidhi vifaa vya hosipitali vilivyotolewa na benki ya NMB kwa kwa Hospitali
ya Mwananyamala .Vifaa hivi vyenye thamani ya shilingi milioni tano
vilikabidhiwa hivi karibuni katika viwanja vya Hospitali hiyo. Akishuhudia
makabidhiano haya ni Meneja wa NMB Tawi la Msasani Bi.Mary Ngallawa.
Meneja wa
NMB tawi la Msasani Bi. Mary Ngallawa Pamoja na Maofisa wa Hospitali ya
Mwananyamala wakiyafurahia mashuka yaliyotolewa na benki ya NMB kwa
ajili ya kupunguza uhaba wa mashuka unaoikabili Hospitali hiyo.
Comments