Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha
maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam zimeonekana kuleta madhara
makubwa kwa wakazi wake na hivyo kuwalazimu baadhi ya watu kuhama kwa
muda kwenye makazi yao huku wafanyaniashara wakilazimika kufunga fremu
zao kutokana na maji mengi kuingia.
Blogu ya Larrybway91 imeweza kunasa
hali halisi ya maeneo mbalimbali yaliyokumbwa na dhahama hiyo ya
mvua. ikiwemo maeneo ya Mbezi Beach, Mwenge, Mikocheni, Lugalo,
Magomeni na Kariakoo. Tazama picha hapo chini.
Mto Kawe unaotenganisha Mbezi Beach na Lugalo.
Katika picha ni daraja linaunganisha Mwenge na Lugalo.
Hali inatisha mwenge.Fremu za biashara zilizopo eneo la Mwenge zikiwa zimefungwa kutokana na mvua kubwa inayoendelea knyesha.
Foleni barabara ya New Bagamoyo, eneo la Bamaga Mwenge.
Unaweza ukasema ni filamu, ila ndio hali halisi, kijana akijaribu kumnususru mwanadada aliyetaka kusombwa na majiUmoja ni nguvu, ilibidi asaidiwe na wasamaria wema.
Barabara ya mwai Kibaki eneo la Mikocheni kwa nyerere.Mikocheni kwa Nyerere Hali halisi ya Mikocheni kwa Nyerere hii leo.
Daraja
linalounganisha mkoa wa pwani na Dar es salaam baada ya kusombwa na
maji na hivyo kuwapa adha wasafiri wanaotumia daraja hilo hasa wale
wanaotokea Bagamoyo kuingia jijini Dar es salaam.
Comments