Penzi ni kikohozi kulificha huliweza, Diamond na bebi ake
Wema Sepetu wamelidhihirisha hilo baada ya madamu(Wema) kumsindikiza
sukari ya warembo(Diamond) mpaka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius
Nyerere ‘JNIA’ wakati akielekea Lagos, Nigeria kwa ajili ya kufanya
video na wasanii wakubwa nchini humo na kuhudhuria event ya Femia Kuti .
Diamond ameondoka Tanzania Machi 30 akiwa na meneja wake,
babu Tale kwa ndege ya shirika la Ethopian Airline. Staa huyo wa kibao
cha ‘My Number one’ aliweza kushea na mashabiki wake kwenye mitandao ya
kijamii baadhi ya picha za kabla na baada ya kufika Nigeria.
Comments