William Malecela akijadili jambo na Mkurugenzi wa Skylight band ili kuweka mambo sawa kabla ya Mwili wa marehemu kuwasili.
Baadhi ya waombolezaji wakibadilishana mawazo Katikati ni Mwanamuziki wa Skylight band Joniko Flower
Waombolezaji
wakiendelea kubadilishana mawazo wakati wakisubili mwili wa marehemu
Kufika,Mwenye Baibui nyeusi ni mke wa Chicago Matelephone na wanamuziki
wa Skylight band
Mkurugenzi wa Skylight Band akijadili jambo na Aneth Kushaba ili kuweka mambo sawa kabla ya Mwili wa marehemu kuwasili.
Mchungaji
wa kanisa alipokuwa Anasali marehemu akiongoza ibada ya kumuombea
Marehemu Ayoub Songoro maaru Chill challa aliyekuwa mwanamuziki na mpiga
Gita wa Skylight Band.
MPIGA
gitaa wa bendi ya Skylight, aliyefariki juzi katika Hospitali ya
Muhimbili jijini Dar es Salaam, Chiri Challa, amezikwa katika makaburi
ya Mwananyamala kwa Kopa, Kinondoni jana na kuhudhuriwa na wadau
mbalimbali.
Awali uongozi wa bendi hiyo
kupitia kwa Meneja wake, Aneth Kushaba ‘AK47’, ulieleza kuwa mwanamuziki
huyo alifariki kutokana na ugonjwa wa kupooza nusu ya mwili wake, hali
iliyosababisha kutofanya kazi ipasavyo.
Kushaba alibainisha kuwa kupooza
huko kulisababisha mishipa ya damu kichwani kupasuka na kumsababishia
maumivu makali sehemu za kichwani.
“Tunatoa pole kwa familia ya
marehemu na mashabiki wetu wote katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa
mpendwa wetu,” alisema Kushaba.
Comments