PICHA : MPIGA GITA WA SKYLIGHT BAND CHIRI CHALLA AZIKWA JIJINI DAR ES SALAAM

 Waombolezaji wakiwa msibani Jana kushoto mwenye tisheti nyeusi ni Mratibu wa Skylight Band
William Malecela akijadili jambo na Mkurugenzi wa Skylight band ili kuweka mambo sawa kabla ya Mwili wa marehemu kuwasili.
Baadhi ya waombolezaji wakibadilishana mawazo Katikati ni Mwanamuziki wa Skylight band Joniko Flower
Waombolezaji wakiendelea kubadilishana mawazo wakati wakisubili mwili wa marehemu Kufika,Mwenye Baibui nyeusi ni mke wa Chicago Matelephone na wanamuziki wa Skylight band
Mkurugenzi wa Skylight Band akijadili jambo na Aneth Kushaba ili kuweka mambo sawa kabla ya Mwili wa marehemu kuwasili.
Gari iliyobeba Mwili wa marehemu Chill Challa likiwasili Nyumbani kwa marehemu
Ndugu na Jamaa wakishusha Mwili wa marehemu Chili Challa
Mwili wa Marehemu ukishushwa kwa ajili ya ibada
Mchungaji wa kanisa alipokuwa Anasali marehemu akiongoza ibada ya kumuombea Marehemu Ayoub Songoro maaru Chill challa aliyekuwa mwanamuziki na mpiga Gita wa Skylight Band.
Misa ya kumuombea Marehemu akiendelea Nyumbani kwake Mwananyamala
Mke wa marehemu akiwa na majonzi
Meneja wa bendi Ya Skylight Aneth Kushaba akiaga mwili wa marehemu
Waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu
Ndugu wa Marehemu wakiweka Shada la maua
MPIGA gitaa wa bendi ya Skylight, aliyefariki juzi katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam, Chiri Challa, amezikwa katika makaburi ya Mwananyamala kwa Kopa, Kinondoni jana na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.
Awali uongozi wa bendi hiyo kupitia kwa Meneja wake, Aneth Kushaba ‘AK47’, ulieleza kuwa mwanamuziki huyo alifariki kutokana na ugonjwa wa kupooza nusu ya mwili wake, hali iliyosababisha kutofanya kazi ipasavyo.
Kushaba alibainisha kuwa kupooza huko kulisababisha mishipa ya damu kichwani kupasuka na kumsababishia maumivu makali sehemu za kichwani.
“Tunatoa pole kwa familia ya marehemu na mashabiki wetu wote katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wetu,” alisema Kushaba.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI