Chama Cha Mapinduzi- London – Uingereza kinaridhia
Salaam za CCM Makao Makuu kuungana na Wakristo- Watanzania na
Ulimwenguni kote kuwatakia kila la kheri na fanaka katika
kusherehekea Sikuu Kuu ya PASAKA 2014.
Aidha CCM
UK inayo imani kubwa kuwa Sherehe hii ya Pasaka itakuwa kigezo cha
kuwakaribisha Watanzania wa Imani zote kujitazama kwa wongufu na
kuridhia misingi mikuu ya Uhuru, Muungano wetu na Umoja wa Taifa letu.
CCM
UK inaungana na Watanzania wote kukememea dhidi ya vichocheo vya aina
zote vinavyohatarisha umoja wa TAIFA LETU, usalama wa raia na mali zao,
uhuru wao wa kuabudu na kusujudu ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Kwa
kuwa Dhamira kuu ya Pasaka ni kujenga Upendo, Mshikamano, Umoja na
Uhuru, hasa katika kipindi hiki cha kutafakari mchakato wa Kupata KATIBA
MPYA yenye kukidhi kiu ya maendeleo kwa Wananchi Kiuchumi na
kimaendeleo kama Taifa moja, CCM UK inawatakia kila la kheri katika
kusheherekea sikukuu hii muhimu kwa Wakristo wote Duniani kwa Amani na
Utulivu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Imetolewa na Abraham Sangiwa - Idara ya Siasa na Uenezi.
CCM – TAWI LA UINGEREZA - UNITED KINGDOM.
20th April -2014
Comments