Afisa Uhusiano Manispaa ya Ilala Bi. Tabu
Shaibu akiwaeleza waandishi wa Habari (hawapo pichani)kuhusu mpango wa serikali
wa kuendelea kuimarisha Masoko katika Jiji la Dar es Salaam, Wakati wa Mkutano
uliofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Afisa Masoko wa Manispaa hiyo Bw. Athuman Mbelwa.
====== ==== ======
Na Frank Mvungi- Maelezo
Serikali yaimarisha masoko 18 katika jiji
la Dar es salaam katika kukabiliana na Ongezeko la Mahitaji ya Wananchi. Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano wa
Manispaa ya Ilala Bi Tabu Shaibu wakati wa mkutano nawaandishi wa habari leo jijini
Dar es salaam.
Akifafanua Bi Shaibu amesema masoko makubwa
ni 5 ambayo ni
Buguruni,Ilala,Ferry,Kisutu na Mchikichini ambapo jumla ya wafanyabiashara wanaotumia masoko hayo ni 8,432.
Akieleza
zaidi Bi Shaibu alimesema kutokana na Utafiti uliofanywa na Ofisi ya
Biashara ya Manispaa ya Ilala mwaka 2009,ilibainika kuwa jumla ya
wafanyabishara 21,500 hawana maeneo ya kufanyia biashara na wanatumia hifadhi
ya barabara na maeneo yasiyoruhusiwa kufanya biashara.
Kutokana na hali hiyo Bi Shaibu alibainisha
kuwa katika bajeti ya 2013/2014 jumla ya
sh.Milioni 240 zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa mabanda ya masoko ya Pugu
,Kigogo fresh,Kiwalani na Kinyerezi ambapo wakandarasi wameshaonyeshwa maeneo
ya ujenzi kwa njia ya zabuni.
Katika hatua nyingine Bi shaibu alisema sh.
Milioni 170 zimetumika kuboresha soko la Samaki feri kwa ajili ya ujenzi
wa zoni ya kukaangia samaki baada ya
kuungua. Pia sh. Milioni 75 zilitumika. kuboresha
mifereji ya maji taka,ukarabati wa meza 23 za kunadia samaki,kuzibua mitaro ya maji
taka na maji ya mvua.
Ni jukumu la wafanyabiashara wote
kuzingatia usafi kwa kuhakikisha kuwa taka zinazozalishwa katika masoko yote
zinahifadhiwa katika maeneo husika na kutunza mazingira ya maeneo ya masoko ili
kuwalinda watumiaji wa huduma zinazotolewa katika maeneo hayo.
Comments