SIMBA NA YANGA 1-1 TAIFA, AZAM YAILAZA JKT RUVU 1-0 CHAMAZI
BAO
la Simon Msuva dakika ya 86, jioni hii limeinusuru Yanga SC kulala
mbele ya mahasimu wake, Simba SC baada ya kupata sare ya 1-1 katika
mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam, wakati Uwanja wa Azam Complex, Chamazi bao la Brian Umony
limeipa Azam ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Ruvu.
Himid Mao akiwatoka wachezaji wa JKT Ruvu leo Chamazi |
Simba
SC ilitangulia kupata bao kupitia kwa Haroun Chanongo dakika ya 68 na
kwa matokeo hayo, Azam inamaliza Ligi Kuu na pointi 62 wakati Yanga SC
inamaliza na pointi 56 katika nafasi ya pili- kwa maana hiyo Azam FC ni
mabingwa wasiopingika wa Ligi Kuu 2013/2014. HABARI ZAIDI ITAFUATIA.
Comments