Ofisa Mkazi
wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Brien Holden Vision, Eden
Mashayo akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana kuhisina
na uzinduzi wa upimaji macho utakao fanyika Dar es Slaam free market
mkabala na kituo cha DSTV , Kinondoni jijini Dr es Salaam. Kushoto ni
Mratibu mradi huo Violet Shirima.
Ofisa Mkazi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Brien Holden Vision, Eden Mashayo akionesha miwani itakayozinduliwa.
********
MKUU
wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika ufunguzi wa utoaji wa huduma ya macho bure, itakayofanyika Dar es
Slaam free market mkabala na kituo cha DSTV , Kinondoni jijini Dr es
Salaam.
Ofisa
Mkazi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Brien Holden Vision, Eden
Mashayo alisema hayo jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari.
Alisema
wameamua kutoa huduma hiyo bure kwa sababu inakadiriwa, watanzania
Milioni 3.5 wameathirika na ugonjwa wa macho wengi wao ni wenye umri wa
miaka 40 na kuendelea.
Alisema
huduma hiyo itaanza kutolewa leo hadi Aprili 11 mwaka huu jijini Dr es
Salaam, kuhamasisha watu kuwa na desturi ya kupima macho mara nyingi
zaidi.
‘’Tumeandaa miwani
za aina 12 ambazo saizi zote zinapatikana na tutaziuza kwa bei
nafuu kuliko wanavyouza mawakala wengine’’ alisema Mashayo.
Comments