TIMU YA SHINDANO LA KUSAKA VIPAJI VYA KUIGIZA LIJULIKANALO KAMA TANZANIA MOVIE TALENTS YAWASILI SALAMA MKOANI DODOMA TAYARI KWA ZOEZI LA USAILI LITAKALOANZA NA PROMOTION PARTY NDANI YA CLUB 84 HAPO KESHO


Hatimaye kikosi kazi cha Proin Promotions Limited kimeshawasili mkoani Dodoma tayari kwa Kazi ya Kusaka vipaji vya kuigiza Katika Kanda ya Kati ambayo inawakilishwa na Mkoa wa Dodoma. Shindano hili linaendelea ambapo awali lilianzia Kanda ya Ziwa Mkoani Mwanza na hatimaye kupatikana kwa washindi watatu wa kanda ya Ziwa huku wakisubiri washindi wa Kanda nyingine kupatikana Kwaajili ya fainali kubwa itakayofanyika Mkoani Dar Es Salaam na mshindi mmoja kuibuka na Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania.
Timu nzima ya Proin Promotions Limited ambao ndio waratibu na waendeshaji wa Shindano hili tayari wapo sawa kwa shughuli hiyo katika kanda ya kati. Zoezi la kusaka Vipaji vya Kuigiza katika Kanda ya Kati itafanyika Mkoani Dodoma ambapo litaanza tarehe 12 Aprili 2014 katika Ukumbi wa African Dreamz uliopo Area C Mjini Dodoma.
Mpaka Sasa kanda zilizobakia ni Kanda ya Juu Kusini  ambapo Mkoa utakaowakilisha ni Mbeya, Kanda ya Kusini  usaili utafanyika Mkoani Mtwara, Kanda Pwani usaili utafanyika Mkoa Dar Es Salaam na Kanda ya Kaskazini usaili utafanyika katika Mkoa wa Arusha huku Mkoa wa Kigoma ukipewa upendeleo wa kuiwakilisha Kanda ya Ziwa tena ambapo tayari zoezi hilo ndipo lilipoanzia Mkoani Mwanza.
Kabla ya Usaili wa kusaka Vipaji vya Kuigiza Kuanza Siku ya Ijumaa kutakuwa na Promotion Party itakayofanyika Katika Ukumbi wa Disco wa 84 kuanzia saa tatu usiku na kuendelea Wakazi wa Kanda ya Kati wanashauriwa kujitokeza kwa wingi kwaajili ya kuonyesha Vipaji vyao na kuitumia fursa hii katika kukuza vipaji vyao

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.