Timu ya watoto wa mtaani kutoka Tanzania iliyoibuka mabingwa wa dunia katika mchezo wa soka yapokewa kishujaa
Mwenyekiti wa Timu ya watoto wa mitaani ya
jijini Mwanza Alfat Mansoor (Dogo) akizungumza na waandishi wa habari mara
baada ya timu hiyo kuwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jana
jijini Dar es Salaam.
Mchezaji aliyesabibisha timu ya watoto wa
mitaani kutoka Tanzania kuibuka mabingwa wa Dunia kw kufunga magoli matatu kwa
mojadhidi ya Burundi Frank William(mwenye kofia nyekundu) akiwa na baadhi ya
wachezaji wenzake mara baada ya juwasili airport,kushoto ni Hassan
Jaffar,Emmanuel Amos, na Hassan Seleman.
Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo
Bi. Juliana Yassoda akiwa amebeba kombe la ubingwa dunia mara baada ya kupokea
timu ya watoto wa mitaani kutoka Tanzania iliyochukua ubingwa huo kwa kuifunga
timu kutoka Burundi jumla ya magoli 3-0. Timu hiyo imewasili nchini jana majira
ya saa 9:35 mchana na kulakiwa na uongozi wa Serikali na wadau mbalimbali wa
soka.
Wachezaji wa timu ya watoto wa mitaani ya
Tanzania ilyo nyakuwa ubingwa wa dunia katika mashindano yaliyofanyika nchini
Brazil kwa kushirikisha timu za watoto wa mitaani, wakiwa wamebeba makombe
waliyoyapa katika mashindano hayo.
Afisa Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Frank Shija akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya wachezaji wa timu ya watoto wa mitaani.Picha zote na Frank Shija, Afisa
Mawasiliano Serikalini, WHVUM
Comments