Uingereza ndani ya Tamasha la Pasaka

  MUIMBAJI wa Kimataifa raia wa Uingereza Ayobami David  ni mmoja wa waimbaji watakaoshiriki katika Tamasha la Pasaka linalotarajia kuanza Aprili 20 katika mikoa nane hapa nchini. Ayobami ni muimbaji ambaye anafanya vizuri katika muziki huo wa Kumtukuza Mungu kupitia nyimbo mbalimbali.

Awali Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Alex Msama ilijipambanua kwamba tamasha la mwaka huu wanatoka kivingine ili kuendana na kasi ya Sayansi na Teknolojia kwa kuwashirikisha waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania. Kwa mujibu wa Msama kwa kuwa wameamua kukuza muziki huo hapa nchini, dhana hiyo itafanyika kila kona ya dunia ili Tanzania ipige hatua zaidi katika tasnia ya muziki huo.

Msama alisema miaka iliyopita walikuwa wakiwatumia katika matamasha yake yaliyoasisiwa tangu mwaka 2000, waimbaji kutoka Kenya, Zambia, Afrika Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na  kwingineko. “Niliyoeleza mwanzoni yanakamilika, kwa sababu nilidhamiria kuliboresha zaidi Tamasha la Pasaka kwa kuwashirikisha waimbaji wa Kimataifa, mashabiki wakae mkao wa kula kupata ladha tofauti katika tamasha la mwaka huu,” alisema Msama.  

Aidha Msama alisema mbali ya Ayobami, Kamati imemuongeza muimbaji wa injili raia wa Rwanda, Lilliane Kabaganza ingawa bado taratibu zinaendelea kuwapata waimbaji wengine wa kimataifa. Mbali ya waimbaji hao wa Kimataifa, wengine ni Rebecca Malope, Keke Phoofolo (Afrika Kusini), Ephraim Sekereti (Zambia), Faraja Ntaboba (DRC) na Sarah K, Paul Mwai (Kenya).Baadhi ya waimbaji wa Tanzania waliothibitishwa kushiriki katika tamasha hilo ni pamoja na John Lisu, Rose Muhando, Upendo Nkone na Upendo Kilahiro.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA