UNHWA YA KOREA KUSINI KUISAIDIA NIMR KATIKA UGUNDUZI WA DAWA KWA KUTUMIA MIMEA




 Na Father Kidevu Blog, Dar es Salaam
Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu Tanzania (NIMR), imesaini mkataba wa ushirikiano na kampuni ya UNHWA ya Jamhuri ya Korea ambapo kampuni hiyo itaisaidia NIMR teknolojia mpya ya kufanya ugunduzi wa dawa za binadamu kwa kutumia mimea.

Makubaliano hayo yamesainiwa jijini Dar es salaam pembezoni mwa kongamano la 28 la kisayansi la NIMR, ambapo mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Dk. Mwele Malecela amesema hatua hiyo ni muhimu katika shughuli za utafiti wa afya nchini na maendeleo ya taasisi kwa ujumla.

Dk. Mwele amesema teknolojia hiyo itaongeza uwezo wa kiwanda cha taasisi cha kutengeneza dawa kwa kutumia mimea kilichopo eneo la Mabibo External jijini Dar es salaam na kwamba itawezesha taasisi kujikita zaidi katika utengenezaji wa dawa za saratani mbalimbali pamoja na za kusaidia udhibiti wa virusi vya ukimwi.

Kwa upande wake afisa mtendaji mkuu wa kampuni hiyo ya NHWA bw. YOUNG WOO JIN amesema kampuni yake imefikia hatua hiyo kutokana na mchango wa NIMR katika masuala ya tafiti na ugunduzi wa dawa ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo katika kiteknolojia ili kuiongezea uwezo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.