Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza na Baadhi ya
Wafanyakazi wa chumba cha habari cha Clouds Media wakati wa Ziara ya
Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari. Kulia ni Mhariri
Mkuu wa Clouds Media Joyce Shebe na Kushoto ni Mhariri wa Habari za
Michezo Shaffih Dauda.
Mhariri
Mkuu wa Clouds Media Joyce Shebe akieleza jambo wakati wa Ziara ya
Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Kituo hicho katikati ni Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene na Kushoto ni Mhariri wa
Habari za Michezo Shaffih Dauda.
Mhariri
wa Picha wa Clouds Media Joachim Kanyopa akimueleza jamabo Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene wakati wa Ziara ya
Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari.
Mtaalam
wa Sauti na Taa wa Clouds Media Cyprian Kisheto akimueleza jamabo
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene wakati wa Ziara
ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari.
=========== ======== =========
Na Jovina Bujulu-MAELEZO.
Wamiliki
wa Vyombo vya habari nchini wametakiwa kutumia waandishi wa habari
wenye Taaluma ya habari ili kuweza kuilinda taaluma hiyo. Wito
huo umetolewa na Mkurungenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah
Mwambene wakati wa Ziara ya Kikazi aliyoifanya katika Kituo cha Clouds
Media leo Jijini Dar es Salaam.
Mwambene
Alisema kuwa kumekuwa kukiongeza kwa wimbi la wanahabarti wasio na
taalum hali inayosababisha kudharaulika kwa taalum hiyo.
“me
napenda kuwaasa wamiliki wa vyombo vya habari kuendelea kusisitiza
uajiri wa watu wenye taalum husika na wale waliosomea masuala haya ya
uandishi wa habari ikiwa ni njia ya kuimarisha na kuilinda taaluma hii”
Alisema Mwambene.
Akizungumzia
kuhusu waandishi wasio uwezo Mhariri Mkuu wa habari Bi. Joyce Shebe
alisema kuwa baadhi ya vyuo vya habari nchini vimekuwa vikizalisha
waandishi wasiokidhi viwango. Aidha
aliongeza kuwa ofisi yao imekuwa na utaratibu wa kuwaendeleza
wafanyakazi kwa lengo la kuwajendgea uwezo wa utendaji kazi katika
Tasnia ya Habari nchini.
Ili
kuhakikisha Tasnia ya Habari inakuwa wadau wa habari nchini wameombwa
kuendelea kuishauri serikali katika masuala mbalimbali yatakayosaidia
kuimarisha Tasnia hiyo.
Comments