Wamiliki wa Vyombo vya habari watakiwa kuheshimu taaluma ya habari



 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza na Baadhi ya Wafanyakazi wa chumba cha habari cha Clouds Media wakati wa Ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari. Kulia ni Mhariri Mkuu wa Clouds Media Joyce Shebe na Kushoto ni Mhariri wa Habari za Michezo Shaffih Dauda.
Mhariri Mkuu wa Clouds Media Joyce Shebe akieleza jambo wakati wa Ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Kituo hicho katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene na Kushoto ni Mhariri wa Habari za Michezo Shaffih Dauda.
 Mhariri wa Picha wa Clouds Media Joachim Kanyopa akimueleza jamabo Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene wakati wa Ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari.
Mtaalam wa Sauti na Taa wa Clouds Media Cyprian Kisheto akimueleza jamabo Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene wakati wa Ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari kwenye Vyombo vya habari.
===========    ========  =========
Na Jovina Bujulu-MAELEZO.

Wamiliki wa Vyombo vya habari nchini wametakiwa kutumia waandishi wa habari wenye Taaluma ya habari ili kuweza kuilinda taaluma hiyo. Wito huo umetolewa na Mkurungenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene wakati wa Ziara ya Kikazi aliyoifanya katika Kituo cha Clouds Media leo Jijini Dar es Salaam.

Mwambene Alisema kuwa kumekuwa kukiongeza kwa wimbi la wanahabarti wasio na taalum hali inayosababisha kudharaulika kwa taalum hiyo.

“me napenda kuwaasa wamiliki wa vyombo vya habari kuendelea kusisitiza uajiri wa watu wenye taalum husika na wale waliosomea masuala haya ya uandishi wa habari ikiwa ni njia ya kuimarisha na kuilinda taaluma hii” Alisema Mwambene.

Akizungumzia kuhusu waandishi wasio uwezo Mhariri Mkuu wa habari Bi. Joyce Shebe alisema kuwa baadhi ya vyuo vya habari nchini vimekuwa vikizalisha waandishi wasiokidhi viwango. Aidha aliongeza kuwa ofisi yao imekuwa na utaratibu wa kuwaendeleza wafanyakazi kwa lengo la kuwajendgea uwezo wa utendaji kazi katika Tasnia ya Habari nchini.

Ili kuhakikisha Tasnia ya Habari inakuwa wadau wa habari nchini wameombwa kuendelea kuishauri serikali katika masuala mbalimbali yatakayosaidia kuimarisha Tasnia hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*