WANANCHI JIMBO LA CHALINZE KUMCHAGUA MBUNGE WAO LEO


BAADA ya kampeni zilizodumu kwa mwezi mmoja, hatimaye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo, Pwani unatarajiwa kufanyika leo ili kumpata mrithi wa Said Bwanamdogo aliyefariki dunia Januari 22 mwaka huu kutokana na maradhi.

Katika kipindi chote cha kampeni, vyama vitano vilichuana kumwaga sera na usiku na mchana katika Kata 15 za jimbo hilo, kila kimoja kikiamini ndicho kitaibuka mshindi na hatimaye kutoa mrithi wa Bwanamdogo.
Vyama hivyo ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachowakilishwa na Ridhiwani Kikwete, Chadema ambacho mwakilishi wake ni Mathayo Torongey na Chama cha Wananchi (CUF) kinachowakilishwa na Fabian Skauti.
Vingine ni AFP ambacho mpeperusha bendera wake ni Ramadhani Mgaya na NRA kinachowakilishwa na Munir Hussein.
Kwa mujibu wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Chalinze ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo, Christina Njovu, maandalizi yote ya uchaguzi huo mdogo yamekamilika.
Alimwambia mwandishi jana kuwa, Jimbo la Chalinze lina vituo vya kupigia kura 288 ambavyo pia vilitumika katika uchaguzi wa mwaka 2010 na kwamba wasimamizi wa uchaguzi wako tayari kwa kazi hiyo, huku akisisitiza waliojiandikisha na kutambuliwa katika daftari la wapiga kura katika jimbo hilo ni wapiga kura 92,588.
Naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei amesema na kutahadharisha wananchi watakaopiga kura kufanya hivyo na baadaye kuondoka eneo la kupiga kura umbali wa zaidi ya meta 100.
Alisema kazi ya ulinzi na usalama katika vituo vyote ni kazi ya jeshi la polisi na sio mtu ama kikundi chochote kiwe cha siasa ama sio cha siasa na iwapo hilo litazingatiwa uwezekano wa upigaji kura na utangazaji matokeo ukawa wa amani na utulivu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI