BRAZIL NA UJERUMANI KUVAANA NUSU FAINALI, UFARANSA NA COLOMBIA ZATUPWA NJE

Beki wa kati wa timu ya Taifa ya Ujerumani, Mats Hummels, ameweka rekodi mpya kwa timu yake baada ya kuifungia goli pekee la ushindi mnamo dakika ya 13′ ya kipindi cha kwanza dhidi ya Ufaransa na kuiwezesha kutinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo kwa mara ya nne mfululizo.
Matokeo hayo yanaifanya Ufaransa kuaga mashindano ya kombe la Dunia huku Ujerumani ikijiandaa kuvaana na wenyeji wa michuano hiyo, timu ya Taifa ya Brazil Julai 08 mwaka huu.
Mats Hummels
Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ujerumani, Mats Hummels, akishangilia mara baada ya kuifungia timu yake bao pekee na la ushindi dhidi ya Ufaransa
Mtanange mwingine uliopigwa hapo jana ni ule uliowakutanisha wenyeji Brazil walioipa kipigo cha bao 2 – 1 Timu ya Taifa ya Colombia katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Estadio Castelao na kushuhudiwa na marais wa mataifa yote mawili.
Mlinzi wa kati wa Brazil anayechezea klabu ya PSG ya Ujerumani, Thiago Silva aliweza kuiandikia timu yake bao la kuongoza mnamo dakika ya saba na kufuatiwa na David Luiz aliyeipatia Brazil bao la ushindi kabla ya Straika wa kutumainiwa wa Colombia, James Rodriguez kufunga bao moja kwa mkwaju wa penalti dakika ya 80′ ambalo halikuweza kugeuza matokeo hayo.
Luiz
David Luiz akishangilia kwa hisia baada ya kuipatia timu yake ya Brazil bao la ushindi
Neymar Jr
Jana Bahati haikuwa ya Neymar Jr baada ya kufanyiwa madhambi na mchezaji wa Colombia hali iliyompelekea atolewe nje kama anavyoonekana katika picha hapo juu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU