Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe akililalamikia kampuni la simu za viganjani Voda Com katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Njombe leo kuhusu kudaiwa kumdanganya Rais Jakaya Kikwete katika uzinduzi wa mtambo wa 3G Njombe. (picjha na Francis Godwin)
Na Francis Godwin Njombe
MBUNGE wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ametaka serikali ya mkoa wa Njombe kuuweka kitomoto uongozi wa kampuni ya simu za viganjani Voda Com kutokana na kudaiwa kumganganya Rais Dr Jakaya Kikwete kuzindua mnala wa 3G ambao haufanyi kazi kwa uwezo wa 3G.
Akizungumza jana katika kikao cha kamati ya Ushauri mkoa (RCC) mkoa wa Njombe mbunge huyo alisema kuwa iwapo uongozi wa mkoa wa Njombe utashindwa kuliweka kitimoto kampuni hilo la Voda Com kwa hatua yake ya kudanganya wananchi wa Njombe na kumdanganya Rais kwa upande wake atalifikisha suala hilo bungeni Dodoma.
Kwani alisema kuwa kati ya maeneo ambayo mtandao wa Voda unasumbua katika upande wa Intarnet ni pamoja na Njombe mjini ambapo mtandao upo taratibu zaidi ukilinganisha na Ludewa ambako hakuna huduma ya 3G.
Hivyo aliwataka wahusika wa mtandao huo kuangalia uwezekano wa kusema ukweli badala ya kudanganya na kuwa kitendo cha Rais kudanganywa ni aibu kwa uongozi wa mkoa mzima wa Njombe .
:"Nitakuwa kiongozi wa mwisho katika mkoa wa Njombe kulifumbia macho suala hili la udanganyifu lililofanywa na kampuni hiyo ya Voda Com na iwapo mkoa utashindwa kuwaita kwa muda unaotakiwa basi yeye kama mbunge atalifikisha suala hilo bungeni ila bunge kutoa kauli "
Mbunge Filikunjombe alisema zipo jitihada mbali mbali zinazofanywa na makampuni ya simu katika kusogeza mawasiliano vijijini kwa wananchi ila ni vizuri makampuni hayo kueleza ukweli kwa wananchi juu ya huduma za mawasiliano
Aidha alisema kuwa ni vema Voda Com kufika mjini Njombe na kuangalia tatizo la wateja wake waliopo umbali wa mita takribani 20 hadi 100 kukosa huduma hiyo ya 3G ili kulifanyia marekebisho
Katika hatua nyingine mbunge huyo aliitaka serikali ya mkoa wa Njombe kurejesha ada katika shule za msingi kuliko kuendelea kuwasumbua wazazi kwa michango isiyokwisha ambayo ni kero kubwa kwa wananchi.
Alisema kuwa iwapo serikali inataka kuboresha elimu ni vizuri kuwe na utaratibu mzuri wa kuchangisha michango kwa wazazi kuliko kuwadanganya wananchi kuwa ada imefutwa huku michango ikiendelea kuwa mingi kuliko hata ada.
Pia alisema kama ada imefutwa basi mkoa kuweka utaratibu mzuri wa michango ambayo itajulikana kwa wananchi wote ili waweze kujipanga
Mwisho
Na Francis Godwin Njombe
MBUNGE wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ametaka serikali ya mkoa wa Njombe kuuweka kitomoto uongozi wa kampuni ya simu za viganjani Voda Com kutokana na kudaiwa kumganganya Rais Dr Jakaya Kikwete kuzindua mnala wa 3G ambao haufanyi kazi kwa uwezo wa 3G.
Akizungumza jana katika kikao cha kamati ya Ushauri mkoa (RCC) mkoa wa Njombe mbunge huyo alisema kuwa iwapo uongozi wa mkoa wa Njombe utashindwa kuliweka kitimoto kampuni hilo la Voda Com kwa hatua yake ya kudanganya wananchi wa Njombe na kumdanganya Rais kwa upande wake atalifikisha suala hilo bungeni Dodoma.
Kwani alisema kuwa kati ya maeneo ambayo mtandao wa Voda unasumbua katika upande wa Intarnet ni pamoja na Njombe mjini ambapo mtandao upo taratibu zaidi ukilinganisha na Ludewa ambako hakuna huduma ya 3G.
Hivyo aliwataka wahusika wa mtandao huo kuangalia uwezekano wa kusema ukweli badala ya kudanganya na kuwa kitendo cha Rais kudanganywa ni aibu kwa uongozi wa mkoa mzima wa Njombe .
:"Nitakuwa kiongozi wa mwisho katika mkoa wa Njombe kulifumbia macho suala hili la udanganyifu lililofanywa na kampuni hiyo ya Voda Com na iwapo mkoa utashindwa kuwaita kwa muda unaotakiwa basi yeye kama mbunge atalifikisha suala hilo bungeni ila bunge kutoa kauli "
Mbunge Filikunjombe alisema zipo jitihada mbali mbali zinazofanywa na makampuni ya simu katika kusogeza mawasiliano vijijini kwa wananchi ila ni vizuri makampuni hayo kueleza ukweli kwa wananchi juu ya huduma za mawasiliano
Aidha alisema kuwa ni vema Voda Com kufika mjini Njombe na kuangalia tatizo la wateja wake waliopo umbali wa mita takribani 20 hadi 100 kukosa huduma hiyo ya 3G ili kulifanyia marekebisho
Katika hatua nyingine mbunge huyo aliitaka serikali ya mkoa wa Njombe kurejesha ada katika shule za msingi kuliko kuendelea kuwasumbua wazazi kwa michango isiyokwisha ambayo ni kero kubwa kwa wananchi.
Alisema kuwa iwapo serikali inataka kuboresha elimu ni vizuri kuwe na utaratibu mzuri wa kuchangisha michango kwa wazazi kuliko kuwadanganya wananchi kuwa ada imefutwa huku michango ikiendelea kuwa mingi kuliko hata ada.
Pia alisema kama ada imefutwa basi mkoa kuweka utaratibu mzuri wa michango ambayo itajulikana kwa wananchi wote ili waweze kujipanga
Mwisho
Comments