KUNDI LA WAPIGANAJI WA KIISLAM LAAGIZA WANAWAKE WOTE KUANZIA MIAKA 11 HADI 46 NI LAZIMA WAKEKETWE.

 
ISIS yaagiza wanawake wote kuanzia umri wa miaka 11-46 kukeketwa.
Umoja wa Mataifa umeelezea ghadhabu kutokana na Fatwa iliyotolewa na Kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa ISIS ya kuwataka wanawake wote waliozidi umri wa miaka 11 kukeketwa.
 
Afisa wa shirika la umoja wa mataifa nchini Iraq ,Jacqueline Badcock ameonya kuwa agizo hilo la kidini ama Fatwa itawaathiri zaidi ya wanawake milioni nne kati ya umri wa miaka 11-46.
Kundi hilo la wapiganaji wa Kiislamu ndilo linaongoza mashambulizi katika maeneo ya Kaskazini mwa Iraq na wao ndio wanaotawala mji wa Mosul.


Kundi hilo linalosheheni wapiganaji wa dhehebu la Sunni ndilo linaloendeleza wimbi la mashambulizi katika taifa hilo linalotishia kusambaratika katika ya maeneo yanayotawaliwa na madhehebu.


Ukeketaji sio kawaida nchini Iraq.

Mapema juma hili, Isisi iliwalazimisha Wakriso katika mji wa Mosul kuondoka na kuandika herufi N kwenye nyumba zao, hatua ambayo imetambuliwa kama kutaifisha mali za Wakristo katika eneo hilo.


Kulingana na amri hiyo mpya iliyotolewa chini ya Sharia, , wanawake wote kati ya umri wa miaka 11 na 46 wanapaswa kukeketwa.
ISIS yaagiza wanawake wote kuanzia umri wa miaka 11-46 kukeketwa.
Bi Badcock alisema kuwa utamaduni huo ni jambo geni sana nchini Iraq na ni swala linalopaswa kujadiliwa.


Alisema hayo alipokuwa akiwahutubia waandishi wa habari kupitia simu ya video katika mji mkuu wa Mkoa wa Kurdi wa Ibril.


Zoezi hilo la kuwapasha tohara wanawake limeenea sana katika mataifa mengi ya Afrika mashariki ya kati na jamii kadhaa barani Asia.


Baraza la Umoja wa mataifa lilipitisha mswada mnamo mwaka wa 2012 ya kuharamisha tamaduni hiyo ya upashwaji tohara kwa wanawake.


Isis ilitwaa mji wa Mosul mnamo mwezi wa Juni miongoni mwa miji mingine midogo midogo kuelekea mji mkuu wa Baghdad.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA