MABOMU YA MACHOZI YALAZIMIKA KUTUMIKA KUWATAWANYA WANANCHI WALIOVAMIA NA KUANZA KUCHOTA MAFUTA KWENYE LORI LA MAFUTA BAADA YA KUPATA AJALI MKOANI IRINGA
Ajali
hiyo imetokea jana eneo la msitu wa serikali wa Saohil wilayani Mufindi
kwenye barabara kuu ya Iringa –Mbeya ambapo watu wawili walijeruhiwa
kwenye ajali hiyo.
Polisi wamelazimika
kutumia mabomu kuwatawanya wananchi hao ambao walikuwa wakiendelea
kumiminika kutaka kuiba mafuta kwenye lori hilo ili kuwaepusha na hatari
ambayo ingeweza kutokea kama lori hilo lingeshika moto.
Mashuhuda wamesema
chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa tairi ya mbele ya lori la mizigo
lililokuwa linatokea mkoani Mbeya na hivyo kukosa mwelekeo na kuligonga
gari la kubeba mafuta lililokuwa linatokea mkoani Iringa na kuanguka.
Comments