MABOMU YA MACHOZI YALAZIMIKA KUTUMIKA KUWATAWANYA WANANCHI WALIOVAMIA NA KUANZA KUCHOTA MAFUTA KWENYE LORI LA MAFUTA BAADA YA KUPATA AJALI MKOANI IRINGA


Jeshi la polisi mkoani Iringa limetumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi ambao walivamia na kuanza kuchota mafuta kwenye lori la kubeba mafuta baada ya kupata ajali. 

 
Ajali hiyo imetokea jana eneo la msitu wa serikali wa Saohil wilayani Mufindi kwenye barabara kuu ya Iringa –Mbeya ambapo watu wawili walijeruhiwa kwenye ajali hiyo.
 
Polisi wamelazimika kutumia mabomu kuwatawanya wananchi hao ambao walikuwa wakiendelea kumiminika kutaka kuiba mafuta kwenye lori hilo ili kuwaepusha na hatari ambayo ingeweza kutokea kama lori hilo lingeshika moto.
 
Mashuhuda wamesema chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa tairi ya mbele ya lori la mizigo lililokuwa linatokea mkoani Mbeya na hivyo kukosa mwelekeo na kuligonga gari la kubeba mafuta lililokuwa linatokea mkoani Iringa na kuanguka.
 
Jeshi la polisi mkoani iringa limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo unaendelea.

 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.