Na Francis Godwin Blog
DIWANI wa chama cha Tanzania Labour Party
(TLP) kata ya Lupingu wilaya ya Ludewa mkoani Njombe John Kiowi
amempongeza mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kwa jitihada zake
anazozifanya katika kuwapelekea maendeleo wananchi wa Ludewa huku
akiwashangaa wapinzani wanaopinga jitihada mbali mbali zinazofanywa na
serikali ya chama cha Mapinduzi (CCM) na kudai kuwa yeye si mpinzani wa
uchwara wa kupinga maendeleo .
Akizungumza na wanahabari jana wakati wa
zoezi la mbunge Filikunjombe na diwani huyo kushiriki na wananchi wa kata
ya Lupingu kuchimba mashimo ya nguzo za umeme na kusimika nguzo hizo za
umeme , Kiowi alisema kuwa ni zaidi ya wabunge watano wamepata
kuliongoza jimbo hilo la Ludewa ila ni mara yake ya kwanza kuona mbunge
akishiriki bega kwa bega na wananchi wake kuchimba mashimo kama ambavyo
mbunge huyo anafanya .
" Jamani wananchi kwanza ni jambo la kumpongeza
mbunge wetu mbali ya kuhimiza wananchi ila mwenyewe pia amekuwa mstali wa
mbele katika kushiriki tofauti na wana siasa wengine ambao muda wote wao ni
watu wa majukwaani ila vitendo sifuri .....nasema Ludewa imempata mbunge na
niweke wazi hapa mimi sio mpinzani hivi tujiulize wenyewe nikisema mimi ni
mpinzani napinga nini hapa haya maendeleo ni kwa faida yangu na wananchi
wote sasa kama mbunge wa CCM wanafanya kuna haja ya upinzani hapa
"
Kiowi alisema kuwa ataendelea kufanya kazi na
mbunge Filikunjombe ikiwa ni pamoja na kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM
katika kata yake kwani chama chake cha TLP katika kata ya Lupingu
kinatekeleza ilani ya CCM ambacho ndicho chama kilichopo madarakani na
peke yake bila kumtegemea mbunge hawezi kufanya lolote.
Diwani Kiowi ambae alikuwa amevalia sare za
CCM katika shughuli hiyo ya maendeleo alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa
yeye si mpinzani ila ni mpenda maendeleo hata sare za CCM zinazotolewa na
mbunge Filikunjombe amekuwa akizivaa na amekuwa mstali wa mbele kumpongeza
mbunge huyo kutokana na kuwa mbunge wa mfano kwa kufanya kazi bila na makundi
yote .
Hata hivyo diwani huyo alisema kuwa katika suala
la maendeleo hata kuwa tayari kuona watu wachache wakimkwamisha mbunge huyo
kwa kushindwa kuunga mkono jitihada zake katika kuwaletea maendeleo na kudai
kuwa kwa upande wake anaona wapinzani ni wana CCM wenyewe wasiopenda
kujivunia maendeleo makubwa mbayo mbunge Filikunjombe ameyapeleka Ludewa
.
Kwa upande wake mbunge Filikunjombe mbali ya
kumpongeza diwani huyo wa TLP kwa kushiriki vema katika shughuli za
maendeleo bado alisema kuwa ni wapinzani wachache nchini ambao wanajitoa
kama diwani huyo katika shughuli za maendeleo zinazoitishwa na mbunge wa CCM
Alisema yapo baadhi ya maeneo wabunge ama madiwani wa
upinzani wamekuwa ni watu wa kupinga kila jambo linalofanywa na mbunge ama
diwani wa CCM na wengine wasiokuwa na uzalendo na Taifa wamefikia hatua ya
kubeza hata jitihada zinazofanywa na Rais Dr Jakaya Kikwete katika kuliletea
maendeleo Taifa jambo ambalo si la kizalendo hata kidogo na kuwa huo si
upinzani wa kweli.
" Nataka kusema hivi wakati wa kampeni ndio wakati
wa kupingana kisera ila baada ya chaguzi hakuna haja ya kuendelea kupingana
ni kuwa wamoja na kuwaletea wananchi maendeleo hivi hebu niulize ujenzi huu
wa barabara ya Lupingu ,Ludewa na Njombe Ludewa unaoendelea ni kwa faida ya
nani hii barabara inatumiwa na wana CCM pekee mbona hata wapinzani mnapita
katika barabara hiyo hiyo sasa unapinga nini wakati huu wa CCM kutekeleza
ilani yake ....tuwe na uzalendo wa nchi yetu tusiwe wa kupinga kila kitu
na mimi nikueleze wazi kama ungejaribu kupinga mradi huu wa umeme kwa
kutoshiriki tungeonana wabaya mbele ya safari"
Akielezea mradi huo wa umeme Filikunjombe alisema
kuwa kwa kasi ambayo wananchi wanaenda nayo katika kujitolea nguvu zao
kuchimba mashimo na kusogeza nguzo katika mashimo hayo ni wazi mradi huo wa
umeme utakamilika kabla ya Desemba mwaka huu .
Aidha alisema kuwa wakati akiingia madarakani mwaka
2010 ni kijiji kimoja pekee cha jimbo hilo la Ludewa ambacho kilikuwa na
umeme wa mafuta ila sasa zaidi ya vijiji 10 vina umeme na kuwa hadi sasa
jumla ya vijiji 49 vitafikiwa na mradi wa umeme huo ambao unatekelezwa kwa
nguvu za serikali ya Tanzania , Swedeni na kanisa na Romani Katoliki Dayosisi
ya Njombe.
|
Comments