Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua bomba la maji wakati wa uzinduzi wa
mradi wa maji Bweni wilayani Pangani mkoa wa Tanga leo.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na mbunge wa Pangani Mhe.Saleh Pamba
wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa maabara
katika shule ya sekondari Kipumbwi huko Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga
leo.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia fukwe za mji wa Pangani wakati
akivuka kwenda kata ya Bweni kwa kutumia kivuko kipya M.V.Pangani
jana.Mji wa Pangani uko katika hatari ya kumezwa na bahari kutokana na
kuongezeka kwa kina cha maji kulikosababishwa na mabadiliko ya tabia
nchi.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mwenyeji wake mkuu wa mkoa wa Tanga
Mhe.Chiku Galawa wakivuka mto Pangani kwa kutumia kivuko kipya
M.V.Pangani kwenda kata ya Bweni ambapo alizindua mradi wa maji,maabara
na kuhutubia mkutano wa hadhara. Picha na Freddy Maro.
Comments