RAIS KIKWETE ZIARANI PANGANI MKOA WA TANGA

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua bomba la maji wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Bweni wilayani Pangani mkoa wa Tanga leo.
 ais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtwika ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa Bweni Wilayani Pangani wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji huko Bweni Wilayani Pangani Mkoa wa Tanga leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na mbunge wa Pangani Mhe.Saleh Pamba wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa maabara katika shule ya sekondari Kipumbwi huko Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia fukwe za mji wa Pangani wakati akivuka kwenda kata ya Bweni kwa kutumia kivuko kipya M.V.Pangani jana.Mji wa Pangani uko katika hatari ya kumezwa na bahari kutokana na kuongezeka kwa kina cha maji kulikosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mwenyeji wake mkuu wa mkoa wa Tanga Mhe.Chiku Galawa wakivuka mto Pangani kwa kutumia kivuko kipya M.V.Pangani kwenda kata ya Bweni ambapo alizindua mradi wa maji,maabara na kuhutubia mkutano wa hadhara. Picha na Freddy Maro.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA