NYOTA
wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo anaendelea kujifariji baada ya
kutolewa Kombe la Dunia kwa kula raha na mpenzi wake, Irina Shayk.
Akiwa
ameshindwa kuisaidia Ureno iliyotolewa hatua ya makundi Kombe la Dunia
nchini Brazil, ameposti picha akiwa na mpenzi wake Irina Shayk wake nje
ya helikopta asubuhi ya leo wanajiandaa kupanda chombo hicho kwenda
kwenye matanuzi.
Ronaldo
ambaye wiki iliyopita aliposti picha akiwa na Irina, leo ameposti picha
hiyo akiwa nje ya helikpota akiambatanisha na ujumbe usemao; 'safari
asubuhi'.
Mapozi: Cristiano Ronaldo (kushoto) awali aliposti picha hii akiwa na 'mupenz', mwanamtindo wa Urusi, Irina Shayk kulia
Wakati
Mwanasoka huyo Bora wa Dunia anakula bata, mpinzani wake mkubwa, nyota
wa Barcelona, Lieonel Messi anaendelea kutesa uwanjani akiwa ameiwezesha
Argentina kutinga Fainali Kombe la Dunia, baada ya kuitoa Uholanzi kwa
penalti 4-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120.
Sasa
Messi anaingia kwenye jaribio la kutwaa Kombe la kwanza la Dunia
atakapoiongoza Argentina katika Fainali Jumapili dhidi ya Ujerumani.
Mambo uwanjani: Lionel Messi anaendelea kutesa katika Kombe la Dunia, wakati Ronaldo anajifariji kwa starehe
Comments