Vifo kutokana na Ebola ni zaidi ya 600

 


Vifo zaidi ya 600 vimetokana na Ebola huko Afrika Magharibi.

Shirika la Afya Duniani WHO linasema kuwa idadi ya watu wanaofariki kutokana na mkurupuko wa maradhi ya Ebola katika maeneo ya Afrika magharibi, sasa imepanda na kufikia zaidi ya watu 600.
Yamkini watu wengine 68 wamefariki katika kipindi cha juma moja lililopita.
Maofisa wa matibabu wa kimataifa na wale wa maeneo hayo wanajaribu kuyafikia maeneo ya mataifa yaliyothirika na ugonjwa huo kama vile Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Changamoto zachelesha udhibiti wa Ebola Afrika Magharibi
Uvumi, wasiwasi,imani potovu na kutoaminiana kunachochea kusambaa kwa ugonjwa huo huku baadhi ya wanaviji huenda wangali wanawaficha wagonjwa wao kwa hofu ya kutengwa.
Ebola ni ugonjwa hatari unaosambaa kwa kasi mno hivyo huenda idadi kamili ya vifo vinavyotokana na Ebola isijulikane.
Baadhi ya waliowahi matibabu sahihi mapema wamepona.

 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU