Mkazi
Kijiji cha Lundusi Kata ya Peramiho wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma,Bibi
Scholastica Mhagama amesema miaka mingi ameishi maisha dhiki na
kunyanyaswa bila msaada kutoka kwa jamii anayoishi hali ambayo imemfanya
amuombe Mungu amchukuwe ili azikwe kwenye jeneza alilojiandalia.
Kila
siku naomba Mwenyezi Mungu anichukue haraka ili nikapumzike kutokana na
mateso ninayoyapata, lakini hofu yangu nikifa je, nitazikwa kama
binadamu wengine? Ndiyo maana nimeamua kujitayarishia jeneza langu
anasema Scholastica Mhagama (76) mwenye ulemavu wa viungo anayeishi pekee yake katika kibanda kilichoezekwa kwa nyasi.
Comments