- Get link
- Other Apps
Joto
la ushindani kati ya wasanii wa Tanzania linazidi kupanda huku
mashabiki na vyombo vya habari wakidaiwa kuchochea kuni kwa namna moja
au nyingine.Diamond
Platinumz ambaye ndiye msanii anaekabiriwa na ushindani mkubwa zaidi
kwa sasa kwa kuwa yuko mstari wa mbele zaidi wa mafanikio katika muziki
hapa nchini na kuvuka mipaka kuiwakilisha Tanzania, amewashauri wasanii
wanaotaka kushindana nae kutojikita katika ushindani wa nyumbani.
Diamond
alifunguka katika mahojiano aliyofanya na The Jump Off ya 100.5 Times
Fm na Jabir Saleh kabla hajapokea tuzo ya AFRIMMA kama mwimbaji bora wa
kiume Afrika Mashariki.
“Tutanue
mawazo, tuache mawazo ya kushindana wenyewe kwa wenyewe Tanzania. Labda
kuleta mabadiliko yataleta mabadiliko ya Chalinze, mababadiliko ya Dar
es Salaam au wapi. ‘Tukakomeshana tukikutana kwenye show labda ya Mwembe
Yanga,’ tuache hizo fikra.” Alisema Diamond.
“Kwa
sababu sisi tunaweza tukafikiri hapa kuna pesa nyingi sana lakini
hakuna pesa nyingi kama ukifirikia kule mbele. Kwa sababu mbele unaweza
kupiga show mpaka dola 100,000 ambayo ni kama milioni 160 au 170. And
that’s the only way we can make a lot of money.
“Nafikiria
huu ni wakati wetu sisi, tufocus sasa na mbele kuliko kufocus hapa
tunakuwa tunabishana sehemu ambayo ni padogo. Hapa tu kwenye chumba
kimoja tunang’ang’ania humuhumu, huyu kashika mlango hatoki…wakati huku
kuna sebule kuna nini…”Aliongeza.
Mkali
huyo wa MdogoMdogo ameeleza kuwa wakati akiwa katika tuzo za BET
alikuwa anaona jinsi ambavyo baadhi ya watu walivyotengeneza makundi na
kuanza kumdiss bila sababu. Lakini yeye kwake hiyo huwa inampa nguvu
zaidi ya kuwaza kuwa ni muda wa kuwakomesha kwa kutoa vitu vikali zaidi.
Comments