KESI YA "MTOTO WA BOKSI" YABADILISHIWA HAKIMU



Washtakiwa watatu wanaokabiliwa na mashtaka ya mauaji dhidi ya mtoto Nasra Rashid Mvungi, wamelazimika kubadilishiwa hakimu baada ya hakimu wa awali, kupata dharura na kutokuwepo mahakamanani hapo.
  
Washtakiwa hao ambao kesi yao imekuwa ikifikishwa na kutajwa, mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro, Mary Moyo, walilazimika kupandishwa kizimbani mbele ya hakimu Agripina Kimanze na kusomewa mashtaka yao, baada ya hakimu moyo kutokuwepo mahakamani, ambapo tofauti na nyakati zingine, shauri hilo lilichelewa kuanza.
  
Mwendesha mashtaka wa polisi Aminatha Mazengo, akisoma shitaka, aliiambia mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kwamba jalada bado lipo kwa mwanasheria mkuu wa serikali, hivyo kuiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo.
  
Mahakama iliridhia ombi hilo, na kupanga Agosti 20 mwaka huu, kufikishwa tena kwa kesi hiyo kwaajili ya kutajwa, kutokana na mahakama hiyo kukosa uwezo kisheria kusikiliza shitaka la mauaji na washtakiwa kurudishwa rumande kutokana na kesi hiyo kutokuwa na dhamana.
  
Kesi hiyo ya mauaji inawakabili washitakiwa watatu akiwemo baba mzazi wa mtoto Nasra, bw. Rashid Mvungi pamoja na waliokuwa walezi wake, Bi Mariam Said na mumewe Mtonga Omary, ambao awali walikuwa wakikabiliwa na shitaka la kula njama na kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto Nasrah Mvungi kabla ya baadaye mashitaka yao kubadilishwa na kuwa ya mauaji baada ya mtoto huyo kufariki dunia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*