MAGUFULI AKAGUA MIZANI YA KISASA YA VIGWAZA MKOANI PWANI PAMOJA NA UJENZI WA BARABARA YA KIBAMBA-KWEMBE-MAKONDEKO (17KM) ITAKAYOPITA KATIKA CHUO KIKUU CHA MUHIMBILI, MLOGANZILA, KIBAMBA
Mhandisi
kutoka Wakala wa Barabara Nchini TANROADS Ndugu Kileo akimuonesha
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli jinsi Mzani mpya wa
Vigwaza utakavokuwa ukipima magari wakati yakitembea tofauti na mizani
mingine nchini.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia kazi ya ujenzi inayofanyika
katika Chuo Kikuu cha Muhimbili kilichopo katika eneo la Mloganzila
Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Dkt. Magufuli alipita hapo
mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Kiwango cha Lami kutoka
Kibamba kwenda Kwembe hadi Makondeko yenye urefu wa Kilometa 17 nje
kidogo ya Jiji la Dar es Salaam
Waziri
wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na baadhi ya
Wakanadarasi wakati wa ziara yake yakutembelea na kukagua ujenzi wa barabara
ya Kiwango cha Lami kutoka Kibamba kwenda Kwembe hadi Makondeko yenye
urefu wa Kilometa 17 nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Comments